• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC awataka wafanyabiashara wa madini kufuata sheria

Posted on: October 16th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Suleiman Mungiya Mzee leo tarehe 11 Septemba, 2022 amekutana na wafanya biashara wadogo wa madini katika Ukumbi wa Uwekezaji uliopo katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara na kuwataka wafanyabiashara hao kufanya biashara kwa kuzingatia sheria na taratibu zilizowekwa na Serikali.

Akizungumza katika kikao hicho, Mheshimiwa Mzee amesema ameshatembelea migodi yote ya madini katika Mkoa wa Mara na kugundua kuwa baadhi ya wafanyabiashara wa madini wanafanya biashara hiyo kiujanja ujanja ili kukwepa kulipa maduhuli stahiki ya Serikali.

“Mkilipa vizuri kodi, mrahaba na ushuru wa huduma itakuwa rahisi kupata huduma za kijamii katika maeneo yenu mnapofanyia biashara ikiwa ni pamoja na barabara, hospitali, maji na shule, na mimi nitahakikisha mnapata huduma bora” alisema Mheshimiwa Mzee.

Mheshimiwa Mzee pia amewataka wafanyabiashara wadogo wote wa madini kukata leseni halali za biashara ili kuwawezesha kuwa huru katika kufanya biashara zao.

Kwa upande wake, Bwana Jakson Ngassa ameiomba Serikali kupitia Benki Kuu ya Tanzania (BOT) kuanza haraka mchakato wa kununua madini ya dhahabu ili wafanyabiashara wa madini wasiathirike na kushuka kwa bei ya dhahabu katika soko la dunia.  

“Hii itatusaidia sisi ambao hatuna mtaji mkubwa kuweza kuhimili ushindani wa kibiashara katika soko la dunia” amesema Bwana Ngassa.

Bwana Ngasa ameeleza kuwa kutoka kwenye uchimbaji soko liko vizuri, lakini katika soko la dunia bei ya dhahabu inacheza sana na wafanyabiashara wengi wanapata hasara kubwa katika hiyo bei.

Aidha, kwa upande wao wafanyabiashara kutoka Mgodi wa Irasanilo uliopo katika eneo la Buhemba, Wilaya ya Butiama wamelalamikia kukosekana kwa mahitaji muhimu katika eneo hilo hususan hospitali.

“Wachimbaji wengi wanapoteza maisha kutokana na umbali kutoka eneo la mgodi hadi ilipo hospitali, na katika uchimbaji ajali zinatokea mara kwa mara” walisema wafanyabiashara hao.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa