• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC awataka viongozi na watendaji Mkoa wa Mara wajitathmini

Posted on: October 7th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Suleiman Mungiya Mzee leo amefungua kikao cha Wadau wa Mfuko wa Maendelea ya Jamii (TASAF) katika Mkoa wa Mara na kuwataka viongozi na watendaji wa Mkoa wa Mara wajitathmini na kujirekebisha kabla hajachukua hatua.

Mheshimiwa Mzee ametoa kauli hiyo baada ya kupokea taarifa ya zoezi la kuwaingiza wanufaika wa TASAF katika mfumo ili waweze kupata malipo yao kupitia benki na simu za mkoanoni katika utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini nchini unaofadhiliwa na TASAF halijaenda vizuri kutokana na changamoto mbalimbali.

“Haiwezekani wanufaika wa mpango huu washindwe kupata fedha kupitia katika simu au benki na Waratibu wa TASAF ngazi ya Halmashauri na Mkoa mpo na mnaileta hapa hoja kama ni changamoto wakati hamjachukua hatua yoyote kuitatua changamoto hiyo” alisema Mkuu wa Mkoa.

Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa amesema anatamani aone kila mmoja anawajibika katika eneo lake na kuachana na visingizio ambavyo havitatui changamoto za wananchi wa Mkoa wa Mara na kuinua maendeleo ya Mkoa wa Mara.

Mheshimiwa Mzee amewaagiza Waratibu wa TASAF katika Halmashauri kuhakikisha kuwa wanufaika wa mpango huo wanasaidiwa kupata vitambulisho au namba za utambulisho kutoka Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA).

Kwa upande wake, Meneja Mtaalamu wa Ufuatiliaji na Uwezeshaji kutoka TASAF Makao Makuu Bibi Salome Mwakigomba ameeleza kuwa TASAF ilianzisha utaratibu wa  kuwalipa wanufaika kutumia taasisi za kifedha ili kuboresha ulipaji wa fedha kwa walengwa wa mpango huo.

Bibi Mwakigomba amewataka Waratibu wa TASAF kuhakikisha kuwa wanufaika wanaingizwa katika mfumo wa malipo ili waweze kupata malipo yao kwa wakati na kupunguza usumbufu wa wananchi kufuata malipo katika vituo vya kulipia.

Aidha, amewataka waratibu wa TASAF kufanyiakazi orodha ya wanufaika wanaotarajiwa kuondolewa katika mfumo baada ya taarifa kuonyesha kuwa wanauwezo wa kujitegemea na kuendesha maisha yao bila ya msaada wa Serikali.

Bibi Mwakigomba amewaomba Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa kusimamia kwa ukaribu utekelezaji wa shughuli za TASAF kwa manufaa ya Halmashauri na wananchi wanaowatumikia katika maeneo yao.

Akizungumza wakati wa kumkaribisha Mkuu wa Mkoa wa Mara, Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Dominicus Lusasi ameeleza kuwa kikao cha leo kilikuwa na lengo la kuwaeleza wadau shughuli za TASAF zilizofanyika; mafanikio ya Mpango yaliyopatikana; changamoto zilizopatikana; na mikakati iliyopo kutatua changamoto hizo.

Aidha, Bwana Lusasi ameeleza kuwa wadau watapata muda wa kufanya majadiliano na hatimae kuwa na mikakati ya pamoja katika kupunguza ama kumaliza kabisa changamoto za utekelezaji wa mpango katika Mkoa wa Mara.

Bwana Lusasi ameeleza kuwa walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini  ni kaya 63,346 zenye idadi ya watu  316,730.

Bwana Lusasi ameeleza kuwa mpango huo una sehemu nne ambazo ni uhawalishaji wa fedha kwa kaya masikini unaofanyika kupitia kutoa ruzuku kwa kaya maskini na kutoa ajira za muda kwa watu wanaotoka kaya masikini; kuongeza kipato kwa kaya maskini kupitia uwekaji wa akiba na shughuli za kiuchumi; kujenga na kuboresha miundombinu ya sekta za Afya, Elimu na Maji; na kujenga uwezo katika ngazi zote za utekelezaji.

 Kikao hicho kilihudhuliwa na Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa, Makatibu Tawala wa Wilaya, Wakuu wa Idara na Vitengo kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, Waurugenzi wa Halmashauri, Waratibu wa TASAF wa Halmashauri na wadau mbalimbali kutoka taasisi za umma na binafsi.  

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa