• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC avitaka vyama vya watu wenye ulemavu kuanzisha miradi

Posted on: February 10th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Sulaiman Mungiya Mzee leo amekutana na viongozi wa vyama vya Shirikisho la Watu wenye Ulemavu (SHIVIWATA) Mkoa wa Mara na kuvitaka vyama hivyo kuanzisha miradi ya uzalishaji mali ikiwa ni sehemu ya kuwakimu watu wenye ulemavu kiuchumi.

Mheshimiwa Mzee ameeleza kuwa Serikali kwa kutambua hali ya watu wenye ulemavu, imetenga fedha kupitia makusanyo ya ndani ya Halmashauri ili kuweza kutoa mikopo kwa ajili ya wananwake, vijana na watu wenye ulemavu.

“Hamuwezi kuwa na vyama vya watu wenye ulemavu ambavyo haviwasaidii wanachama wake, vinapaswa vyama hivi viwe na vyanzo vya mapato ili kuweza kuwapa wanachama wake manufaa yanayokusudiwa” alisema Mheshimiwa Mzee.

Mkuu wa Mkoa ameeleza kuwa bila vyama hivi kujihusisha na shughuli za uzalishaji mali, havitaweza kujiendesha na kuwasaidia wanachama wake inavyotakiwa na havitaweza kuwawezesha watu wenye ulemavu kunufaika na fursa mbalimbali zinazotolewa na Serikali.

“Bila kuwa na shughuli za uzalishaji mali itakuwa vigumu kwa mlemavu mmoja mmoja au hata kwa ujumla wenu kunufaika na fursa hiyo, hivyo ninashauri kwa kuwa tayari mpo katika vyama vya watu wenye ulemavu, vyama hivi vitumike kuwasaidia” alisema Mheshimiwa Mzee.

Aidha, amewataka watu wenye ulemavu kupambana ili kupata maisha bora na kuahidi kuwasaidia kama wataanzisha mradi wowote ambao utakuwa na tija.

Mheshimiwa Mzee pia amewaagiza Maafisa Maendeleo ya Jamii kuwasaidia watu wenye ulemavu kuunda vikundi na kuanzisha miradi kulingana na hali halisi waliyonayo katika maeneo yao na kusaidiwa kupata mikopo ya Halmashauri ili waweze kuanzisha biashara.

Wakati huo huo, Mkuu wa Mkoa ametoa siku saba kwa Halmashauri za Wilaya za Butiama, Rorya, Musoma na Manispaa ya Musoma ambazo hazijazindua Kamati za Watu Wenye Ulemavu katika Halmashauri kuzindua Kamati hizo na kutoa taarifa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Mheshimiwa Mzee ametoa maagizo hayo kufuatia taarifa ya SHIVIWATA kuonyesha kuwa Halmashauri hizo hazijazindua rasmi Kamati za Watu wenye Ulemavu ambazo zipo kwa mujibu wa Sheria.

Wakizungumza katika kikao hicho, viongozi wa SHIVIWATA wamemshukuru Mkuu wa Mkoa wa Mara kwa kukutana nao na kuuomba Mkoa kuwasaidia katika kufanikisha shughuli mbalimbali wanazozifanya kwa ajili ya watu wenye ulemavu.

Kikao hicho kilihudhuriwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Msalika Robert Makungu, Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe Dkt. Zabron Masatu, maafisa Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii na maafisa wengine wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa