• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC atoa siku 20 Musoma DC na Bunda DC kuhamia majengo mapya

Posted on: September 26th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Said Mohamed Mtanda leo (tarehe 23 Septemba, 2023) amefanya ziara katika Halmashauri ya Wilaya ya Musoma na ametoa siku 20 kwa Halmashauri za Musoma DC na Bunda DC kuhamia kwenye majengo mapya ya Halmashauri hizo.

Mhe. Mtanda ametoa agizo hilo baada ya kukagua ujenzi wa jengo la Halmashauri ya Wilaya ya Musoma linaloendelea kukamilishwa katika eneo la Suguti na kuiagiza Halmashauri hiyo kumalizia upande mmoja wa jengo hilo na kuhamia.

“Hili jengo hapa tayari limeshakaa vizuri, unahitajika ukamilishaji wa mambo yaliyobakia na usafi tu jengo lianze kutumika” amesema Mhe. Mtanda.

Aidha, amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo kuhakikisha mawasiliano yanaimarishwa katika jengo hilo ili kuwezesha mifumo yote na wataalamu wote wa Halmashauri hiyo  kuhamia katika eneo la Suguti ili kurahisisha utoaji wa huduma kwa wananchi.

Mhe. Mtanda amewataka wananchi wa eneo la Suguti kuandaa sherehe ya kuipokea Halmashauri yao katika eneo la Suguti na kuitaka Halmashauri hiyo kuhakikisha inahamia katika muda iliyopewa.

Akiwa katika Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Musoma, Mhe. Mtanda amemuagiza Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Miundombinu na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Musoma kuandaa taarifa ya kiasi cha fedha kinachohitajika ili huduma muhimu ziweze kuongezwa katika Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Musoma.

Aidha, Mheshimiwa Mtanda ametoa mwezi mmoja kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma kupeleka shilingi milioni 41 ili kukamilisha ujenzi wa Kituo cha Afya Kiriba ili huduma ziweze kuanza katika kituo hicho.

Mhe. Mtanda amewapongeza wananchi wa Kijiji cha Manyere kwa kujitolea kusaidia ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Manyere kwa kusaidia kusogeza viashiria kama vile mchanga, mawe na kokoto katika eneo la ujenzi wa mradi huo.

Katika ziara hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Mara amekagua ujenzi wa nyumba mbili za walimu (two in one) katika Shule ya Sekondali ya Ifulifu, ujenzi wa Kituo cha Afya Kiriba na ujenzi wa Shule mpya ya Sekondari ya Wanyere.

Aidha,Mkuu wa Mkoa amekagua ujenzi wa jengo la Halmashauri ya Wilaya ya Musoma, kutembelea ujenzi wa  Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Musoma na kukagua huduma zinazotolewa katika hospitali hiyo.  

Katika ziara hiyo, Mkuu wa Mkoa aliambatana na Mkuu wa Wilaya ya Musoma, Kamati ya Siasa ya Wilaya, Kamati ya Ulinzi ya Wilaya, Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii, wawakilishi wa Makatibu Tawala wasaidizi sehemu za Elimu na Miundombinu na viongozi na watendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa