• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC atoa siku 14 wanafunzi wore Sekondari ya J. K. Nyerere wapate chakula shuleni

Posted on: July 28th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo tarehe 28 Julai, 2025 amefanya ziara Wilaya ya Tarime na kumtaka Mkuu wa Wilaya ya Tarime kuhakikisha wanafunzi wote wa Shule ya Sekondari ya J. K. Nyerere iliyopo Nyamwaga, Halmashauri ya Wilaya ya Tarime wanapata chakula cha mchana wakiwa shuleni.

Mhe. Mtambi ametoa agizo hilo wakati akizungumza na wanafunzi wa kidato cha pili wa shule hiyo baada ya kupokea taarifa kuwa wanafunzi wanaosoma kutwa wa kidato cha kwanza hadi cha nne ambao wazazi wao wamechangia chakula tu ndio wanaopewa chakula shuleni.  

“Ninatoa siku 14 Mhe. Mkuu wa Wilaya ya Tarime hakikisha wanafunzi wote wa shule hii ikiwemo na hawa wanaosoma kutwa wanapata chakula cha mchana wakiwa shuleni, hali hii haikubaliki” amesema Mhe. Mtambi.

Aidha, Mhe. Mtambi amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime kutoa chakula cha mchana kwa wanafunzi wote wa kidato cha pili wa shule hiyo wanaoendelea na mtihani wa upimaji wa kidato cha pili Kimkoa ulioanza leo katika Mkoa wa Mara.

“Mkurugenzi wapatie chakula cha mchana hawa wanafunzi wanaofanya mtihani mpaka mtihani wao utakapoisha ili waweze kufanya vizuri katika mtihani wao” ameagiza Mhe. Mtambi.

Akizungumza katika eneo hilo, Mkuu wa Shule ya Sekondari ya J. K. Nyerere Mwalimu Melesiana Julius Gerald amesema kuwa uongozi wa shule pamoja na Halmashauri hiyo umefanya jitihada mbalimbali kuhakikisha wanafunzi wote wanapata chakula shuleni.

Mwalimu Gerald amesema kwa sasa wanafunzi wote wa kidato cha tano na sita ambao wanakaa bwenini wanapata chakula hata hivyo baadhi ya wanafunzi wa kidato cha kwanza hadi cha nne wanaosoma kutwa katika shule hiyo hawapati chakula shuleni.  

“Kwa sasa ni kama robo tatu ya wanafunzi wanaosoma ndio wanapata chakula shuleni na wengine hawapati chakula kutokana na ugumu wa wazazi kuchangia chakula kwa ajili ya watoto wao” amesema Mwalimu Gerald.  

Wakati huo huo, Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo amekabidhi mizinga ya kufugia nyuki 121 iliyotolewa na wadau mbalimbali kwa Baraza la Wazee pamoja na wazee wa mila wa koo 12 za Kabila la Wakurya wa Wilaya ya Tarime na kuwahakikishia wazee kuwa Serikali inauthamini sana mchango wao katika jamii.

Akizungumza katika tukio hilo, Mhe. Mtambi amesema lengo la kuwapa mizinga hiyo ni kuanzisha miradi wa ufugaji nyuki katika misitu iliyopo katika Wilaya ya Tarime jambo ambalo litawaweka wazee hao kuwa karibu na misitu ambayo wamekuwa wakiitunza katika maisha yao yote.

Mhe. Mtambi ametumia fursa hiyo kuwahamasisha wazee hao kushiriki uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 kwa kupiga kura na kuihamasisha jamii kupiga kura ili kupata haki yao ya kikatiba ya kuwachagua viongozi watakaowaongoza katika nafasi mbalibmbali ikiwemo Rais, Wabunge na Madiwani.

Kanali Mtambi amewashukuru wadau wote waliochangia kufanikisha wazee hao kupata mizinga ya kufugia nyuki ambayo itawasaidia kuanzisha mradi wa kuwainua kiuchumi na kuwaeleza kuwa Serikali imeendelea kuboresha upatikanaji wa huduma mbalimbali kwa wazee.  

Aidha, Mhe. Mtambi ambaye katika ziara hiyo ameambatana na Kamati ya Usalama ya Mkoa na Kamati ya Wataalamu wamekagua miradi itakayotembelewa na Mbio za Mwenge wa Uhuru katika Halmashauri ya Wilaya ya Tarime kwa mwaka 2025.  

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC atoa siku 14 wanafunzi wore Sekondari ya J. K. Nyerere wapate chakula shuleni

    July 28, 2025
  • Kusaya apokea ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Butiama

    July 25, 2025
  • Mtambi ataka matumizi ya GOTHOMIS kwa asilimia 100 Mara

    July 25, 2025
  • Mtambi aitaka FEZA kuwekeza Butiama kumuenzi Mwalimu Nyerere

    July 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa