• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC atoa miezi minne kukamilisha ujenzi wa hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Musoma

Posted on: August 6th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi ameitaka Halmashauri ya Wilaya ya Musoma kukamilisha ujenzi wa Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Musoma ndani ya miezi miwili ili iweze kutoa huduma kama ilivyokusudiwa.

Mheshimiwa Hapi ametoa maagizo haya leo tarehe 4 Agosti 2021 wakati alipofanya ziara katika halmashauri hiyo kukagua miradi ya maendeleo katika Halmashauri ya Wilaya ya Musoma.

“Haiwezekani wataalamu mmekaa tu fedha inakuja mpaka inarudi bila kufanyiwa kitu chochote kile, sasa naagiza hadi kufikia mwishoni mwa Desemba 2021 hospitali hii iwe inatumika na hatutakubali tena visingizio,” alisema Mheshimiwa Hapi.

Aidha amemwagiza Mkuu wa Wilaya ya Musoma kuhakikisha ujenzi wa wodi tatu za wagonjwa katika hospitali hiyo ambayo imeletewa fedha miezi sita iliyopita unaanza na unakamilika kwa haraka.

Mheshimiwa Hapi ameitaka SUMA JKT inayojenga mradi wa ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Musoma kufanya kazi usiku na mchana ili kukamilisha kazi hiyo kwa mujibu wa mkataba.

Awali wakitoa taarifa Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wlaya ya Musoma Bwana Frank Magabiro pamoja na Mhandisi wa wilaya Gibai James Maige wameeleza kuwa mradi wa ujenzi wa hospitali hiyo ulianza kutekelezwa mwaka wa fedha 2018/2019.

Hata hivyo mradi huo haukukamilika kwa sababu fedha zake baada ya muda wa matumizi kuisha zilirudishwa serikalini, baadaye zikaletwa tena Mei, 2021 lakini hadi tarehe 30 Juni 2021 fedha hizo hazikutumika zikarudi tena serikalini.

Aidha walieleza kuwa kwa sasa fedha hizo zimeletwa tena na wapo katika mchakato wa kununua vifaa na kuleta maji eneo la ujenzi ili kukamilisha ujenzi huo.

Wakati huo huo hospitali hiyo ilipokea fedha za ujenzi wa wodi tatu za wagonjwa lakini halmashauri imenunua baadhi ya vifaa vya ujenzi na kufyatua matofali lakini ujenzi haujaanza.

Katika ziara hiyo Mheshimiwa Hapi pia alitembelea mradi wa ujenzi wa ofisi ya Halmashauri ya wilaya ya Musoma, miradi ya Shule ya Sekondari ya Msihakamano, Sekondari ya Ufundi ya Musoma na Bandari ya Musoma inayomilikiwa na Mamlaka ya Bandari Tanzania.

Katika ziara hiyo Mheshimiwa Hapi aliambatana na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Albert Gabriel Msovela, Mkuu wa Wilaya ya Musoma Dkt. Alfany Haule, mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Musoma na viongozi wengine.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa