• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC atatua mgogoro wa mpaka Rigicha

Posted on: May 23rd, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo ameanza ziara yake katika Wilaya ya Serengeti ambapo ametatua mgogoro wa mpaka katika Kijiji cha Rigicha na kuwapongeza wananchi wa kijiji hicho kwa kutafuta ufumbuzi wa mgogoro huo kwa kufuata sheria na taratibu.

Akizungumza katika eneo hilo, Mhe. Mtambi amesema wananchi hao wamekuwa ni mfano wa kuigwa katika utatuzi wa migogoro ya ardhi katika Mkoa wa Mara kwa kufuata sheria na maridhiano  ya kifamilia na kijamii.

“Ninaomba niwapongeze sana wananchi wa Kijiji cha Rigicha, kwa busara na ustahimilivu wenu wa kusubiri kuutatua mgogoro huu kwa kufuata misingi ya haki na sheria, hongereni sana” amesema Mhe. Mtambi.

Baada ya kuwasili katika eneo hilo, Mkuu wa Mkoa amewasikiliza wananchi kutoka familia moja ambao walikuwa wanagombea mpaka wa eneo pamoja na maombi ya kuhamisha njia ya muda mrefu ili kuruhusu shamba la familia kuwekewa mipaka.

Mgogoro huo ulitokana na Bi. Magdalena Francis kuomba kuhamisha barabara ya eneo hilo ipite pembezoni ya shamba la familia yake na baadaye kuanzisha mgogoro na Bwana Mgosi Magesa ambaye anapakana naye na kugombea sehemu ya shamba hilo.

Hata hivyo, Mhe. Mtambi amesuluhisha mgogoro huo na kusimamia uwekaji wa mpaka mpya wa barabara katika eneo hilo na kuwataka familia iliyokuwa na mgogoro kushikana mikono kuashiria kuhitimishwa rasmi kwa mgogoro huo.

Baada ya hapo, Mhe. Mtambi amezungumza na wananchi wa Kijiji hicho na kumwagiza Mkurugenzi wa Halmashauri kuongeza watumishi katika Zahanati ya Kijiji cha Rigachi na kuitaka RUWASA kukamilisha mradi wa maji katika eneo hilo.

Kwa upande  wake kiongozi wa familia iliyokuwa na mgogoro wa ardhi Bwana John Francis Kisongo alisema kuwa eneo hilo ni la familia yao na mababu zao walikuwa wanalima wa mashamba hayo  wakati wakiwa hai na wanaogombania sasa ni warithi baada ya wamiliki wa awali kufariki.

Bwana Kisongo amewataka wanafamilia hao kuheshimu mpaka uliowekwa leo katika eneo hilo na kuwaomba kuendelea kuishi kwa amani kama ilivyokuwa awali kabla ya kuanza kwa mgogoro huo.

Baada ya hapo, Mkuu wa Mkoa amekagua mradi wa Maji wa Nyiberekela na kufanya kikao cha ndani na viongozi wa Wilaya ya Serengeti kabla ya kufanya mkutano wa hadhara katika eneo la Isenyi, Kata ya Isenyi na kupokea na kutatua kero mbalimbali za wananchi wa eneo hilo.

Katika ziara hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Mara aliambatana na baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Usalama Mkoa wa Mara, Kamati ya Usalama ya Wilaya ya Serengeti, Mwenyekiti wa Halmashauri na Menejimenti ya Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti, maafisa kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara na Wakuu wa Taasisi za umma zilizopo Wilaya ya Serengeti.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa