• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC atao taarifa ziara ya Waziri Mkuu

Posted on: February 24th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Said Mohamed Mtanda leo ametoa taarifa ya ziara ya Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb.) Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Mkoa wa Mara kuanzia tarehe 25 Februari, 2025 hadi tarehe 29 Februari, 2024.

Akizungumza na Waandishi wa Habari Mhe. Mtanda amesema katika ziara hiyo, Mhe. Waziri Mkuu anategemea kuzungumza na watumishi na viongozi, kufanya mikutano ya hadhara, kutembelea, kukagua, kuweka mawe ya msingi na kuzindua miradi mbalimbali ya Maendeleo katika sekata za  Utawala, Elimu, Afya na miundombinu.

“Maandalizi ya ziara ya Mhe. Waziri Mkuu katika Mkoa wa Mara yamekamilika. Napenda kuchukua fursa hii kuwashukuru wananchi, watumishi na viongozi wa ngazi mbalimbali walioshiriki kwa namna moja au nyingine kufanikisha maandalizi ya ziara ya Mhe. Waziri Mkuu katika Mkoa wa Mara” amesema Mhe. Mtanda.

Mhe. Mtanda amesema mapokezi ya Mhe. Waziri Mkuu kimkoa yatafanyika eneo la Ndabaka, Wilaya ya Bunda tarehe 25 Februari, 2024 mchana na baadaye ataelekea Ukumbi wa Uwekezaji wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara kwa ajili ya kupokea taarifa ya maendeleo ya Mkoa wa Mara.

Mhe. Mtanda ameeleza kuwa tarehe 26 Februari, 2024 Mhe. Waziri Mkuu atasalimia wananchi eneo la Mariwanda kabla ya kutembelea na kukagua Shule ya Msingi Sabasita iliyopo eneo hilo, atakagua na kuweka jiwe la msingi katika mradi wa ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Mkoa wa Mara Halmashauri ya Wilaya ya Bunda. Baada ya hapo Mhe. Waziri Mkuu atakagua na kuzindua mradi wa maji wa Sazira na kufanya kikao na watumishi na viongozi kisha kufanya mkutano wa hadhara katika uwanja wa Shule ya Msingi Miembeni, Bunda Mjini.

Mhe. Mtanda ameeleza kuwa tarehe 27 Januari, 2024 Mhe. Waziri Mkuu atakagua na kuweka jiwe la msingi katika mradi wa ujenzi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Butiama, kufanya kikao na watumishi na viongozi, kuwasalimia wananchi wa Butiama na kutembelea nyumbani kwa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere eneo la Mwitongo, Butiama.

Aidha, Mhe. Waziri Mkuu atafanya kikao na watumishi na viongozi Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti na mkutano wa hadhara katika Uwanja wa Sokoine, Mugumu na baadaye kuweka jiwe la msingi katika ujenzi wa Zahanati ya kijiji cha Getarungu. Mheshimiwa Waziri Mkuu ataelekea Nyamwaga ambapo ataweka jiwe la msingi katika jengo la utawala Halmashauri ya Wilaya ya Musoma na kusalimiana na wananchi.

Mhe. Mtanda ameeleza kuwa tarehe 28 Feburuari, 2024 Mhe. Waziri Mkuu atatembelea na kukagua mradi wa maji Komuge na baadaye kutembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Rorya kabla ya kufanya mkutano wa hadhara katika eneo la Utegi. Baadaye Mhe. Waziri Mkuu atafanya mkutano wa hadhara katika eneo la Sirari na kuweka jiwe la msingi katika ujenzi wa soko la kimkakati la Mji wa Tarime na kufanya mkutano wa hadhara katika Uwanja wa Serengeti katika Mji wa Tarime.

Tarehe 29 Februari, 2024 Mhe. Waziri Mkuu atakagua ujenzi wa Uwanja wa Ndege Musoma ataelekea kijiji cha Suguti kuweka jiwe la msingi katika Ofisi za Halmashauri ya Wilaya ya Musoma na atazungumza na viongozi na watumishi.

Kwa mujibu wa ratiba hiyo, Mhe. Waziri Mkuu ataenda kijiji cha Bwai (Bwai Kumsoma) kwa ajili ya kuzungumza na wananchi katika uwanja katika Kijiji cha Bwai na kuhitimisha ziara yake katika Manispaa ya Musoma ambapo atafanya mkutano wa hadhara katika uwanja wa Shule ya Sekondari Mara.

 Mhe. Mtanda amewaomba wananchi kujitokeza kwa wingi kushiriki katika mapokezi na mikutano ya hadhara iliyopangwa karibu na maeneo yao.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa