• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC Ataka Wadau kusaidia Nyumba Salama

Posted on: January 11th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Suleiman Mungiya Mzee amewaomba wadau wa maendeleo na watu wenye uwezo kuzisaidia Nyumba Salama, vituo vinavyowahudumia watoto waliokimbia vitendo vya ukatili katika jamii ili kuviwezesha vituo hivyo kuwahudumia watoto kwa ufanisi na kuepusha watoto kurudi tena kwenye ukatili.

Mheshimiwa Mzee ametoa wito huo baada ya kupokea taarifa kuwa watoto 70 ambao walikuwa wamekimbilia Nyumba Salama ya AFTGM Masanga iliyopo katika Wilaya ya Tarime wamekeketwa baada ya kurejeshwa majumbani kwao baada ya msimu wa ukeketaji kuisha.

“Hili linatokea kwa sababu hivi vituo havina uwezo wa kutunza watoto wengi kwa muda mrefu na kulazimika kuwarejesha kwa wazazi ambao wanaenda kuwakeketa hata baada ya kuingia makubaliano na vituo hivyo kuwa watawalinda” alisema Mzee.

Mheshimiwa Mzee ameeleza kuwa namna bora ya kuwaepusha watoto kukumbana na ukatili huo ni kuziwezesha Nyumba Salama ili ziweze kutoa huduma kwa muda mrefu zaidi hata baada ya muda wa ukeketaji kuisha.

Mheshimiwa Mzee amesema Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara itatoa shilingi milioni 9 kusaidia Kituo cha AFTGM Masanga, Shirika la Hope for Women and Girls lenye Nyumba Salama mbili za Matumaini katika Wilaya za Butiama na Serengeti na Nyumba Salama ya Kanisa la Anglican Tanzania (ACT Mara).  

Aidha, katika ziara hiyo, Mkuu wa Mkoa aliitisha harambee na kufanikiwa kukusanya mchango zaidi ya shilingi 200,000 kutoka kwa viongozi alioambatana nao na kuukabidhi kwa Msimamizi wa Kituo cha ACT Mara.   

Akizungumza katika ziara hiyo, Mkurugenzi wa Shirika la Hope for Women and Girls Bibi Rhobi Samwel ameeleza kuwa katika kuwatunza watoto wanakutana na changamoto mbalimbali ikiwemo baadhi ya viongozi wa siasa kuwasaidia watu waliokamatwa kwa makosa ya ukeketaji ili waachiwe.

Bibi Rhobi Samwel amepongeza ushirikiano wanaoupata kutoka kwa viongozi mbalimbali wa Serikali katika mapambano dhidi ya ukeketaji na vitendo vingine vya ukatili ikiwemo ndoa za utotoni, vipigo, na ukeketaji.

Kwa sasa Mkoa wa Mara una Nyumba Salama za kuwahifadhi waliokimbia ukatili nne ambazo ni AFTGM Masanga (Tarime), ACT Mara (Serengeti), Matumaini (Serengeti na Butiama).  

Hata hivyo, kutokana na changamoto ya fedha, watumishi, sehemu ya kuishi watoto wengi wanaopokelewa katika vituo hivi hurudishwa baada ya msimu wa ukeketaji kuisha (Agosti- Desemba) hata hivyo kwa mwaka huu ukeketataji unaendelea kufanyika kwa watoto waliokuwa wamekimbia awali.

Katika ziara hiyo, Mkuu wa Mkoa aliambatana na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Mara, Kamati ya Usalama ya Mkoa, Kamati ya Usalama ya Wilaya za Tarime, Serengeti na Butiama, baadhi ya maafisa kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, Menejimenti za Halmashauri ya Wilaya ya Tarime, Serengeti na Butiama.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa