• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC ataka ushirikiano wa viongozi kuleta mabadiliko Mara

Posted on: August 6th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Meja Jenerali Suleiman Mzee leo tarehe 6 Agosti, 2022 amewasili katika Mkoa wa Mara na kuwataka viongozi wa Mkoa huo kushirikiana katika kuleta mabadiliko ya kimaendeleo na kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili wananchi wa Mkoa wa Mara.  

Akizungumza baada ya mapokezi yake yaliyofanyika leo baada ya kuwasili, Mheshimiwa Mzee ameeleza kuwa viongozi wa Mkoa wa Mara wakishirikiana vizuri wananchi watapata maendeleo kwa haraka zaidi.  

“Mimi nitajitahidi kuwa mvumilivu maana Mheshimiwa Rais (Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan) alisema huku ni uraiani, lakini sitakuwa mvumilivu na mtu yoyote anayekwamisha au anayechelewesha miradi ya maendeleo ya wananchi wa Mkoa wa Mara” alisema Mheshimiwa Mzee.

Mheshimiwa Mzee amewaomba viongozi wa Mkoa wa Mara kutoa ushirikiano  katika kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili wananchi.  

“Hapa tupo kwenye ziwa, kilimo chetu bado kinategemea mvua, lakini tukishirikiana tutatafuta ufumbuzi wa kuweza kutumia maji ya ziwa katika kilimo cha umwagiliaji na kuwasaidia zaidi wakulima” alisema Mheshimiwa Mzee.  

Aidha, Mheshimiwa Mzee amewataka viongozi kushiriki kikamilifu katika maandalizi na uhamasishaji wa Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022 ili Mkoa wa Mara uweze kufanya vizuri katika zoezi hilo kwa manufaa ya wananchi na Taifa kwa ujumla.  

“Mimi ninawaomba tushirikiane vizuri katika maandalizi na hususan uhamasishaji wa wananchi katika kushiriki kikamilifu katika zoezi la Sensa ili Sensa ya mwaka huu ifanyike vizuri katika Mkoa wetu” alisema Mheshimiwa Mzee.

Mkuu wa Mkoa amepokelewa na viongozi wa Mkoa wa Mara wakiongozwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Msalika Robert Makungu katika eneo la Ndabaka, Wilaya ya Bunda ambapo ni mpakani kati ya Mkoa wa Mara na Mkoa wa Simiyu katika Barabara ya Mwanza- Musoma- Sirari.

Baada ya mapokezi hayo, viongozi hao walielekea ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara ambapo Mkuu wa Mkoa alisaini kitabu na kuzungumza na viongozi mbalimbali wa Mkoa wa Mara walioshiriki mapokezi hayo.

Viongozi wengine waliokuwepo katika mapokezi hayo ni Wakuu wa Wilaya, Kamati ya Usalama ya Mkoa, baadhi ya viongozi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Mara, Wakuu wa Idara na Vitengo vya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, Makatibu Tawala wa Wilaya na baadhi ya watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Mheshimiwa Meja Jenerali Suleiman Mzee ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mara tarehe 31 Agosti, 2022 kuchukua nafasi ya Mheshimiwa Dkt. Raphael Chegeni aliyeteuliwa tarehe 28 Agosti, 2022 kuchukua nafasi ya Mheshimiwa Ally Salum Hapi ambaye uteuzi wake umetenguliwa.  

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa