• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC ataka mpangokazi Mugango- Kiabakari

Posted on: December 29th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Suleiman Mungiya Mzee leo ametembelea mradi wa Maji wa Mugango- Kiabakari- Butiama na kumtaka Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira Mugango -Kiabakari (MKWSSA) kuwasilisha mpangokazi wa ukamilishaji wa mradi huo ofisini kwake tarehe 30 Desemba, 2022.

Akizungumza wakati wa ukaguzi wa mradi huo, Mheshimiwa Mzee ameeleza kuwa hajaridhiwa na utekelezwaji wa mradi huo ambao awali ulitakiwa ukamilike Desemba 17, 2022 na sasa umeongezewa muda hadi Juni, 2023.

“Tatizo ninaloliona hapa ni Mshauri Mwelekezi wa mradi anaukwamisha mradi kwa kutokujibu mapendekezo ya mkandarasi kwa wakati na kushindwa kuridhia au kukataa kuendelea na hatua inayofuata ya ujenzi, matokeo yake kazi kubwa imekwama” amesema Mheshimiwa Mzee.

Mheshimiwa Mzee amemtaka Mkurugenzi wa MKWSSA kuifahamisha Wizara ya Maji kuhusiana na mapungufu ya Mshauri Mwelekezi wa mradi ili kama inawezekana Wizara isitishe mkataba wake ili mradi uweze kukamilika kwa wakati.  

Mheshimiwa Mzee pia ameelezea wasiwasi wake kuhusiana na malipo ya ziada ambayo mkandarasi anaweza kuja kuidai Serikali baada ya kucheleweshwa kufanyakazi na Mshauri Mwelekezi wa mradi kwa mujibu ya mkataba.

Mkuu wa Mkoa ameahidi kuufuatilia mradi huo mara kwa mara kuanzia sasa ili wananchi wa Wilaya za Musoma na Butiama wanaotarajiwa kunufaika na mradi huo waweze kupata maji safi na salama ya uhakika.

Akizungumza katika ziara hiyo, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani Mheshimiwa Jumanne Sagini amememshukuru Mkuu wa Mkoa kwa kufanya ziara katika mradi huo na kueleza kuwa katika ziara yake ya Mkoa wa Mara amepanga kuutembelea mradi huo.

“Kumekuwa na changamoto kubwa ya maji kwa wananchi wa Butiama baada ya mradi wa zamani kukatiwa maji baada ya mamlaka hiyo kukatiwa umeme na Shirika la Umeme nchini (TANESCO) alisema Mheshimiwa Sagini.

Mheshimiwa Sagini ambaye pia ni Mbunge wa jimbo la Butiama ameahidi kuwasiliana na Wizara ya Maji ili kuweza kutatua changamoto za maji kwa wananchi wa Butiama baada ya wananchi wa eneo hilo kukosa maji.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa MKWSSA Mhandisi Cosmas Sanga ameeleza kuwa mradi wa maji wa Mugango- Kiabakari Butiama una thamani ya shilingi bilioni 70.5 na unajengwa na mkandarasi UNIK Construction Engineering na Mshauri Mwelekezi ni Sajdi Consulting Engineering Center.

Mhandisi Sanga ameeleza kuwa kwa sasa mradi huo umefikia asilimia 71 ya utekelezaji wakati malipo katika mradi huo yamefikia asilimia 58 ya fedha zote.

“Mradi huu ulianza tarehe 17 Desemba, 2020 na ulipaswa kukamilika tarehe 17 Desemba, 2022 lakini kutokana na changamoto ya UVIKO 19 mkandarasi ameomba kuongezewa muda wa miezi sita za utekelezaji wa mradi hadi tarehe 30 Juni, 2023” alisema Mhandisi Sanga.

Mhandisi Sanga ameeleza kuwa mradi huo kwa awamu ya kwanza unahusisha ujenzi wa chanzo cha maji, chujio la maji, jengo la utawala la MKWSSA, nyumba za watumishi, matanki ya maji 7 mapya na ukarabati wa matanki mawili, usafirishaji wa maji na usambazaji wa maji kwa wananchi wa vijiji 16.

Kwa mujibu wa Mhandisi sanga, vijiji vingine 23 vitakavyonufaika na mradi huo mchakato wa zabuni kumpata mkandarasi unaendelea kupitia Wizara ya Maji.   

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa