• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC apokea madarasa 64 Tarime

Posted on: January 6th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Suleiman Mungiya Mzee leo amefanya ziara katika Wilaya ya Tarime na kupokea vyumba vya madarasa 64 vyenye thamani ya shilingi bilioni 1.28 kwa ajili ya kupokea wanafunzi wa kidato cha kwanza mwaka 2023.

Akizungumza katika ziara hiyo, Mheshimiwa Mzee ameipongeza Wilaya ya Tarime kwa usimamizi mzuri wa ujenzi wa madarasa na hususan utengenezaji wa viti na meza kwa ajili ya wanafunzi.

“Ninawapongeza kwa kazi kubwa mliyoifanya katika kusimamia ujenzi wa vyumba vya madarasa na yamekamilika kwa ubora na kwa wakati” alisema Mheshimiwa Mzee.

Mheshimiwa Mzee amewataka watendaji wa Serikali wanaosimamia utekelezaji wa miradi kusimamia utekelezaji wa miradi kwa weledi na ubora unaotakiwa na sio kulipua kazi.

Aidha, amewatahadharisha wazazi ambao hawata wapeleka watoto wao kuanza shule, serikali ya Mkoa wa Mara haitamvumilia mzazi yoyote atakayeshindwa kumpeleka mtoto shule na itamchukulia hatua za kisheria.

Akizungumza katika ziara hiyo, Mbunge wa Tarime Vijijini Mheshimiwa Mwita Waitara ameeleza kuwa anaishukuru sana Serikali kwa kujenga vyumba vya madarasa na Shule mpya mbili katika jimbo lake ambazo zitapunguza msongamano wa wanafunzi madarasani.

Mheshimiwa Waitara ameeleza kuwa kwa mwaka huu wanafunzi wa Kata ya Sirari wanaotarajia kuanza Kidato cha Kwanza ni zaidi ya 700 na awali walikuwa na shule moja tu Sirari Sekondari, kuongezwa kwa shule mpya katika eneo hilo kumesaidia sana.

Amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha za miradi mbalimbali ya maendeleo katika jimbo hilo na Wilaya ya Tarime kwa ujumla.

“Jimbo hili limepata shule mbili mpya moja ya milioni 600 na nyingine ya zaidi ya bilioni moja hizi zitasaidia sana kupunguza michango kwa wananchi ya ujenzi wa vyumba vya madarasa na kuwawezesha watoto kuwa na mazingira bora ya kujifunzia” alisema Mheshimiwa Waitara.  

Akiwa katika Halmashauri ya Mji wa Tarime, Mheshimiwa Mzee ametembelea Shule ya Sekondari ya Bomani, Shule ya Sekondari ya Ikoro na Shule ya Sekondari ya Magena na kuiagiza Halmashauri hiyo kurekebisha baadhi ya mapungufu aliyoyaona na kukamilisha ujenzi wa vyoo katika Sekondari za Ikoro na Magena.

Katika Halmashauri ya Wilaya ya Tarime, Mheshimiwa Mzee ametembelea shule mbili zinazojengwa na Serikali kupitia mradi wa Maendeleo ya Elimu ya Sekondari nchini (SEQUIP) ambazo ni Shule ya Sekondari ya Bukira na Shule ya Sekondari ya Nyasaricho.

Katika ziara hiyo, Mkuu wa Mkoa aliambatana na Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Kamati ya Usalama ya Tarime, Katibu Tawala Msaidizi sehemu ya Elimu, Katibu Tawala Msaidizi sehemu ya Miundombinu, Kaimu Katibu Tawala Msaidizi sehemu ya Mipango na Uratibu , menejimenti za Halmashauri ya Tarime Mji na Halmashauri ya Wilaya ya Tarime.

Wengine walioshiriki ziara hiyo ni mwakilishi wa Katibu wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Tarime, Mbunge wa Jimbo la Tarime Vijijini, Katibu wa Mbunge wa jimbo la Tarime Mjini, madiwani na watendaji wengine.  

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa