• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC akagua ujenzi wa vyumba vy a madarasa

Posted on: November 9th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Suleiman Mungiya Mzee leo amekagua vyumba vya madarasa katika Halmashauri ya Manispaa Musoma, Halmashauri ya Wilaya ya Butiama na Halmashauri ya Mji wa Bunda na kupongeza kazi inayoendelea.

Akizungumza katika maeneo mbalimbali, Mheshimiwa Mzee ameeleza kazi inayoendelea ni nzuri sana na kuwapongeza mafundi na wasimamizi wa miradi hiyo katika ngazi mbalimbali katika ujenzi huo.

“Ninawapongeza kwa kuwa kazi inayofanyika ni nzuri sana, inaonekana hata kwa macho na niwaombe tu tukamilishe kazi hii kwa ubora na wakati” alisema Mheshimiwa Mzee.

Aidha, Mheshimiwa Mzee amewataka Wakurugenzi kujenga ofisi za walimu katikati ya vyumba vya madarasa ili kupunguza tatizo la uhaba wa ofisi za walimu katika Mkoa wa Mara.

Mheshimiwa Mzee pia amelipongeza Jeshi la Magereza kwa kazi nzuri wanayoifanya katika ujenzi wa vyumba vya madarasa wanavyoendelea kujenga katika Halmashauri mbalimbali za Mkoa wa Mara.  

Wakati huo huo, Mkuu wa Mkoa amewataka Wakuu wa Shule za Sekondari kubuni na kuanzisha miradi midogo midogo katika maeneo yao ili kuweza kupata fedha za kutatua changamoto mbalimbali pamoja na kutumika kwa ajili ya mafunzo kwa vitendo kwa wanafunzi.

“Miradi hiyo inaweza kuwapa fedha za kutatua changamoto ambazo bila ya fedha hizo haziwezi kutatuliwa kiurahisi ikiwa ni pamoja na kuboresha mazingira yenu ya kazi” alisema Mheshimiwa Mzee.

Katika Manispaa ya Musoma Mheshimiwa Mzee ametembelea Shule ya Sekondari ya Baruti (madarasa 4) na Shule ya Sekondari ya Morembe (madarasa 4) na kukuta ujenzi ukiwa unaendelea katika hatua za maboma na Jeshi la Magereza likiwa limepatiwa zabuni hizo.

Katika Halmashauri ya Wilaya ya Butiama, Mheshimiwa Mzee ametembelea Shule ya Sekondari ya Mmazami ambayo awali ilipewa vyumba 13 vya madarasa lakini kutokana na uhaba wa eneo, vyumba 06 vinajengwa katika eneo hilo na vyumba 07 vinajengwa katika eneo la Sekondari mpya ya Kirumi.

Katika Halmashauri wa Mji wa Bunda, Mheshimiwa Mzee amekagua Shule ya Sekondari ya Dkt. Nchimbi ambayo imepewa vyumba 10 vya madarasa na kwa sasa ipo katika hatua ya kujenga msingi na ujenzi unatekelezwa na Jeshi la Magereza.

Katika ziara hiyo pia, Mkuu wa Mkoa amezungumza na wanafunzi wa Kidato cha kwanza katika Shule ya Sekondari ya Baruti na kuwataka wanafunzi kujifunza kwa juhudi ili waweze kutumia muda huo kuboresha maisha yao ya baadaye.

Katika ziara hiyo, Mkuu wa Mkoa ameambata na na Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Elimu Bwana Benjamin Oganga, Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Miundombinu Mhandisi Richard Moshi na watumishi wengine kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Wilaya na Halmashauri zilizotembelewa.

Vyumba vya madarasa vilivyokaguliwa leo ni sehemu ya vyumba vya madarasa 546 vinavyojengwa katika shule za Sekondari 144 katika Mkoa wa Mara yenye thamani ya shilingi 10,920,000 kwa ajili ya kupokea wanafunzi wa kidato cha kwanza mwaka 2023.

Mkoa wa Mara umepanga kukamilisha ujenzi wa vyumba vya madarasa hayo mwanzoni wa Desemba, 2022 kabla kufika tarehe ya mwisho iliyowekwa na Serikali ya ukamilishaji wa ujenzi wa vyumba vya madarasa.  

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa