• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC aitaka RUWASA kutoa taarifa ya vyanzo vya maji

Posted on: February 10th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Suleiman Mungiya Mzee leo ameongoza kikao cha kuwajengea uelewa wa pamoja baina ya Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) Mkoa wa Mara na kuitaka Wakala hiyo kuwasilisha taarifa ya vyanzo vya maji na mkakati wa kivilinda vyanzo vilivyopo ofisini kwake kwa ajili ya kupata uelewa wa pamoja wa viongozi ndani ya Mkoa.

“Ninataka nipewe taarifa ya vyanzo vya maji vilivyopo na mkakati wa kivilinda vyanzo hivi ili viongozi wote tuuelewe na tushiriki kulinda kwa ajili ya kuleta uhakika wa maji kwa maendeleo ya wananchi katika Mkoa wa Mara” amesema Mheshimiwa Mzee.  

Mheshimiwa Mzee ametoa agizo hilo baada ya baadhi ya wajumbe wa kikao hicho kulalamika kuwa kuna baadhi ya vyanzo vya maji havijatunzwa vizuri na kusababisha uharibifu wa vyanzo hivyo kutokana na shughuli mbalimbali za kibinadamu.

Mkuu wa Mkoa ameitaka RUWASA kuendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu Sheria ya Huduma ya Maji na Usafi wa Mazingira na. 5 ya mwaka 2019 ili wananchi waepuke kuharibu mazingira na vyanzo vya maji bila kujua kuwa ni kosa kisheria.

Aidha, Mheshimiwa Mzee ameitaka RUWASA kufuatilia miradi ya maji inayotekelezwa katika Mkoa wa Mara ili iweze kukamilika kwa wakati na kutoa huduma ya maji kwa wananchi.

Mheshimiwa Mzee amewataka viongozi waliohudhuria kikao hicho kuwaelimisha wananchi wanaowawakilisha ili kulinda vyanzo vya maji na uharibifu wa mazingira.

Kwa upande wake, Mhandisi wa RUWASA Mkoa wa Mara, Nuni Munjobelege ameeleza kuwa lengo la kikao hicho ni kujenga uelewa wa pamoja baina ya RUWASA, Sekretarieti ya Mkoa na viongozi mbalimbali kuhusu mwelekeo mpya wa utoaji wa huduma yam aji vijijini chini ya Sheria ya Huduma za Maji na Usafi wa Mazingira Na. 5 ya mwaka 2019.

Akizungumza wakati wa kutoa mada kuhusu hali ya utekelezaji wa ujenzi wa miradi ya maji katika Mkoa wa Mara, Mhandisi Nuni ameeleza kuwa kwa sasa miradi yote ya maji inayotelekezwa katika Mkoa wa Mara inaendelea vizuri.

Mhandisi Nuni ameeleza kuwa kwa sasa Mkoa una miradi ya maji 115 inayotekelezwa na vikundi vya watumia maji 91 vinavyoendesha miradi hiyo baada ya baadhi ya vikundi kuanza kuunganishwa ili kuendana na mwongozo mpya wa vikundi vya watumiaji maji katika ngazi ya jamii.

 Kikao hicho kimehudhuriwa pia na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara, Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Mara, Wakuu wa Wilaya, Kamati ya Siasa ya Mkoa, Kamati ya Usalama ya Mkoa, Wakuu wa Idara na Vitengo vya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, Makatibu Tawala wa Wilaya, Wenyeviti wa Halmashauri, Wakurugenzi wa Halmashauri na wakuu wa baadhi ya taasisi za serikali.  

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa