• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC aipongeza Idara ya Afya

Posted on: August 30th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenarali Suleiman Mungiya Mzee leo ameipongeza Idara ya Afya ya Mkoa wa Mara kwa kufanikisha awamu ya pili ya chanjo ya polio kwa Watoto chini ya miaka mitano iliyofanyika hapa nchini kuanzia Mei 18-22, 2022.

Mheshimiwa Mzee ametoa pongezi hizo leo wakati akifungua kikao cha Kamati ya Afya ya Msingi Mkoa wa Mara mahususi kwa ajili ya utekelezaji wa kampeni ya chanjo ya polio yam atone kwa awamu ya tatu inayotarajiwa kuanza tarehe 1-4 Septemba, 2022.

“Katika awamu ya pili Mkoa ulichanja Watoto 630,897 ambao ni sawa na asilimia 119 ya Watoto 529,725 ya Watoto waliotarajiwa kuchanjwa katika Mkoa wa Mara” alisema Mheshimiwa Mzee.

Amewataka viongozi na watendaji wote kuongeza juhudi katika kampeni na utekelezaji wa zoezi la chanjo kwa awamu ya tatu ili Mkoa uweze kufanya vizuri zaidi katika zoezi hilo kwa kutumia fedha zilizopokelewa.

Mheshimiwa Mzee amewaagiza Wakuu wa Wilaya kusimamia awamu ya tatu ya chanjo katika Wilaya zao ili zoezi hili liweze kufanikiwa katika Mkoa wa Mara.

Akizungumza kabla ya kumkaribisha Mkuu wa Mkoa wa Mara, Katibu Tawala Msaidizi Sehemu y Afya Dkt. Juma Mfanga ameeleza kuwa hii ni awamu ya tatu kwa Tanzania kufanya zoezi la chanjo ya polio kwa Watoto wa chini ya miaka mitano baada ya ugonjwa huo kugundulika katika nchi ya Malawi Februari, 2022.

“Kwa awamu ya kwanza ilihusika mikoa michache iliyopo jirani na nchi ya Malawi na awamu ya pili ilikuwa nchi nzima na sasa inafanyika tena nchi nzima kwa watoto wote chini ya miaka mitano” alisema Dkt. Mfanga.

Dkt. Mfanga amewataka wajumbe wa kikao hicho kutoa elimu na kuwahamasisha wananchi waweze kulipokea zoezi hilo vizuri na kutoa ushirikiano kwa maafisa wa chanjo.

Kwa upande wake, Mratibu wa Chanjo Mkoa wa Mara Bibi Flowina Muuzaje ameeleza kuwa Mkoa kwa kushirikiana na Wizara ya Afya, Shirika la Afya Duniani (WHO) na Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto (UNICEF) watafanya kampeni ya siku nne.

Bibi Muuzaje ameeleza kuwa katika kipindi hicho kampeni itafanyika nyumba kwa nyumba na katika maeneo yote yenye watoto wa chini ya miaka mitano ikiwemo vituo vya kutolea huduma za afya kama ilivyofanyika wakati wa awamu ya pili.

Aidha Bibi Muuzaje ameeleza kuwa Mkoa bado unaendelea kutoa elimu kwa umma kupitia vyombo vya habari, mikutano ya wananchi, matangazo, vipeperushi na mitandao ya kijamii.

Kikao cha Afya ya Msingi Mkoa wa Mara kilihudhuriwa pia na Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara, Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri, Waganga Wakuu wa Halmashauri pamoja na maafisa kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa