• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC aipongeza Butiama kwa kupata hati safi na ukusanyaji wa mapato

Posted on: June 27th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo amehudhuria kikao cha Baraza la Madiwani cha kujadili hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali  (CAG) za mwaka 2022/2023 na kuipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Butiama kwa kupata hati safi na ukusanyaji wa mapato ya Serikali.

Mhe. Mtambi ametoa pongezi hiyo katika kikao kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Butiama na kuipongeza Halmashauri hiyo kwa kupata hati safi kwa muda wa miaka minne mfululizo.

“Hii inaonyesha kuwa mifumo ya usimamizi ye Menejimenti ya Halmashauri hiyo na Baraza la Madiwani lipo imara katika kuisimamia Halmashauri katika utekelezaji wa majukumu yake ya kila siku” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi amewataka watendaji wa Halmashauri hiyo kuongeza juhudi na weredi ili Halmashauri iendelee kupata hati safi kwa miaka inayofuata na kuendelea kupunguza hoja za ukaguzi na hususan zinazoweza kupata majibu.

 Aidha, Mhe. Mtambi ameipongeza Halmashauri hiyo kwa kufanikiwa kukusanya shilingi 1,743,111,105 hadi kufikia tarehe 30 Mei, 2024 ambayo ni sawa na asilimia 87.48 ya lengo la makusanyo ya mapato ya ndani kwa mwaka wa fedha  2023/2024.

“Ni imani yangu kuwa kwa kipindi hiki kilichosalia mtafika na kuvuka lengo la makusanyo ya mapato ya ndani ili kuwawezesha kutekeleza mipango ya maendeleo iliyokasimiwa katika kipindi hicho” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi ameitaka Halmashauri hiyo kukamilisha utekelezaji wa maagizo sita ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (LAAC) ya tarehe 21 Juni, 2022 ambayo Halmashauri haijafanikiwa kukamilisha utekelezaji wake na kulitaka Baraza la Madiwani kusimamia uandaaji wa mpango kazi wa kuhakikisha maagizo na hoja zote zinafanyiwa kazi kikamilifu.

Kanali Mtambi amelitaka Baraza la Madiwani kuwawajibisha watumishi wote waliosababisha hoja za ukaguzi na kusimamia ukamilishaji wa miradi viporo iliyopo katika Halmashauri hiyo ili wananchi wapate huduma.

Mhe. Mtambi ameagiza manunuzi yote yafanyike kupitia mfumo wa Manunuzi ya Umma (NEST)  na madiwani na watumishi wote wapewe mafunzo kuhusu mfumo wa NEST, Sheria ya Ununuzi wa Umma ya mwaka 2023 na kanuni zake.

Aidha, amelitaka Baraza la Madiwani kusimamia mgawanyo wa mali na madeni kati ya HAlmashauri ya Wilaya ya Butiama na Halmashauri ya Wilaya ya Musoma.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Butiama Mheshimiwa Moses Kaegele amepongeza ushirikiano uliopo katika ya Baraza la Madiwani, Menejimenti ya Halmashauri na watumishi wote wa Halmashauri unaosaidia katika utekelezaji wa shughuli za maendeleo.

Mhe. Kaegele amesema Halmashauri hiyo kwa sasa imepiga hatua kubwa katika kujibu hoja za CAG na kuwataka wataalamu waendelee kutekeleza majukumu yao kwa mujibu wa Sheria, Kanuni na taratibu ikiwa ni pamoja na kuongeza bidii na ubunifu katika shughuli zao.

Taarifa ya ukaguzi uliofanywa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) katika mwaka wa fedha 2022/2023 Halmashauri hiyo  ilipata hati safi na ilikuwa na hoja 42 kati ya hizo hoja 16 zilikuwa za miaka ya nyuma na hoja za mwaka wa fedha 2022/2023 ilikuwa na hoja 26 huku maagizo sita ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (LAAC).

Aidha, taarifa hiyo imeonyesha kuwa Halmashauri hiyo ilikuwa pia na hoja za mfuko wa wanawake, Vijana na watu wenye ulemavu na hoja za Mfuko wa Afya wa Pamoja (HSBF) ambazo utekelezaji wake bado unaendelea. 

 Taarifa hiyo imeeleza kuwa kati ya hoja zote zilizokuwepo, hoja 16 zimehakikiwa na kufungwa na CAG na kati ya zilizofungwa na hoja 12 ni za mwaka 2022/2023 na hoja nne ni za miaka ya nyuma.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa