• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC Afungua kikao cha Kitaifa cha Maandalizi ya Siku ya Mara

Posted on: August 25th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Suleiman Mzee leo amefungua rasmi kikao cha Kitaifa cha maafisa wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuhusu maandalizi ya Siku ya Mara (Mara Day) ambayo yanatarajia kufanyika tarehe 12-15 Nakuru, nchini Kenya.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa kikao hicho, Mheshimiwa Mzee amewataka maafisa kutoka taasisi mbalimbali zilizohudhuria kikao hicho kutekeleza kwa vitendo maamuzi ya kutunza mazingira katika maeneo yote kuzunguka Mto Mara.

“Mimi ninataka maadhimisho haya yawe yanaacha alama kwa kupanda miti ya kutosha na kulinda miti iliyopandwa ili kuacha alama ya kudumu kwa wananchi wa Mkoa wa Mara” alisema Mheshimiwa Mzee.

Mheshimiwa Mzee pia amewataka maafisa hao kufanya maandalizi mapema ya Siku ya Mara na kutoa hamasa zaidi kwa wananchi kushiriki hususan katika kupanda miti na kutunza miti yote itakayopandwa katika maadhimisho hayo.

Akitoa ufafanuzi kuhusiana na historia ya maadhimisho hayo, Mkurugenzi wa Miundombinu ya Kiuchumi na Huduma za Jamii wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki Bwana Eliabi Khalid Chodota ameeleza kuwa maadhimisho hayo ni utekelezaji wa maamuzi ya Mkutano wa 10 wa Baraza la Mawaziri wa kisekta la Bonde la Ziwa Victoria uliofanyika tarehe 4 Mei, 2012 Kigali, Rwanda.

“Maadhimisho haya hufanyika kwa lengo la kutoa msukumo kwa hifadhi ya bonde la Mto Mara unaoanzia milima ya Mau nchini Kenya na kuishia Ziwa Victoria kwa upande wa Tanzania” alisema Bwana Chodata.

Bwana Chodota ameeleza kuwa maadhimisho haya yamekuwa yakifanyika kuanzia mwaka 2012 kila mwaka na kilele cha maadhimisho hay ani tarehe 15 Septemba ya kila mwaka hii ikihusiana na uhamaji wa Wanyamapori kutoka Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, Tanzania Kwenda Maasai Mara nchini kenya kwa ajili ya malisho na baadaye kurudi kuzaliana katika Hifadhi ya Serengeti.  

Kikao cha Kitaifa cha maandalizi ya Siku ya Mara kilihucdhuriwa pia na Maafisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Wizara ya Uvuvi na Mifugo, Wizara ya Kilimo, Wizara ya Maji, Ofisi za Bonde la Ziwa Victoria na Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.

Wengine waliohudhuria kikao hicho ni Wakuu wa Wilaya, Makatibu Tawala wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri, baadhi ya maafisa wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, Maafisa Mazingira na maafisa Maendeleo ya Jamiiwa Halmashauri za Mkoa wa Mara.

Baada ya kikao hicho, kikao cha kimataifa cha maandalizi ya Siku ya Mara kilifanyika kwa njia ya mtandao na kuwahusisha maafisa kutoka nchi za Kenya, Tanzania na Mashirika ya Kimataifa yanayohusiana na mazingira, maji na uhifadhi.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa