• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC aagiza kukamatwa kwa wazazi ambao hawajapeleka watoto shule

Posted on: January 13th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Suleiman Mungiya Mzee leo amewaagiza Wakuu wa Wilaya zote za Mkoa wa Mara kuanza kuwachukulia hatua za kisheria wazazi wa watoto ambao wanatakiwa kwenda shule lakini hawajapelekwa.

Mheshimiwa Mzee ametoa agizo hilo leo katika eneo la Nyamswa katika Wilaya ya Bunda baada ya kupokea taarifa za usajiri wa wanafunzi usioridhisha katika Wilaya ya Bunda hadi tarehe 11 Januari, 2023.

“Ninataka kuona watoto wote wamepelekwa shule au wazazi wawe wamechukuliwa hatua za kisheria na nipate taarifa ya utekelezaji wa agizo hili” alisema Mheshimiwa Mzee.

Mheshimiwa Mzee amesema haitavumilika kuona Serikali imewekeza fedha nyingi katika ujenzi wa miundombinu ya shule ikiwa ni pamoja na kuweka walimu huku wazazi wakikwamisha jitihada za Serikali za kuboresha elimu hapa nchini.

Aidha, Mheshimiwa Mzee amewaagiza wasimamizi wa elimu katika Mkoa wa Mara kusimamia ufundishaji na ujifunzaji wa wanafunzi wanapoenda shule.

Awali, Mheshimiwa Mzee aliwauliza wanafunzi wa shule za msingi mbalimbali kutoka katika Tarafa ya Chamriho waliohudhuria hafla hiyo maswali ya uelewa na kutoa shilingi 10,000 kwa ambaye angeweza kujibu maswali hayo, lakini hamna aliyeweza kujibu kwa usahihi.

Aidha, Mheshimiwa Mzee amewataka Walimu Wakuu na Wakuu wa Shule kuboresha mazingira ya shule na sehemu nyumba za walimu zilizopo katika mazingira ya shule ili wanafunzi waweze kujifunza sio tu masomo ya darasani lakini hata namna nzuri ya kuishi kwenye mazingira masafi.

“Mwanafunzi akija shule mbali ya masomo anajifunza kutoka kwa walimu na watu wengine wanavyovaa, wanavyoishi, wanavyoongea na wanavyofanya mambo yao, hivyo walimu wakiwa wanaishi katika mazingira ya hovyo, wanafunzi wanakuwa hawana cha kujifunza” alisema Mheshimiwa Mzee.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkuu wa Wilaya ya Bunda Mheshimiwa Joshua Nassari ameeleza kuwa katika Wilaya hiyo usajiri wa wanafunzi ni mdogo katika Halmashauri zote mbili pamoja na Wilaya kuchukua hatua za kuwawezesha wazazi kuwapeleka watoto shule.

“Katika Wilaya ya Bunda tumeruhusu wazazi kuwapeleka watoto shule hata wasipokuwa na sare za shule au michango ya shule ili watoto waweze kuanza masomo yao lakini bado wanafunzi wachache wameandikishwa mpaka sasa” alisema Mheshimiwa Nassari.

Mheshimiwa Nassari ametolea mfano wa Kata ya Nyamswa ambapo kati ya wanafunzi 392 waliotakiwa kuanza kidato cha kwanza, wanafunzi 90 tu walikuwa wamepokelewa shuleni mpaka tarehe 11 Januari, 2022.

Mheshimiwa Nassari ameeleza kuwa katika Wilaya ya Bunda wametoa siku saba wazazi wote wenye watoto wanaotakiwa kwenda shule wame wamepelekwa shule na baada ya hapo wataanza kuchukua hatua za kisheria.

Aidha, Mheshimiwa Nassari ameeleza kuwa katika fedha zilizotolewa mwaka 2022 za ujenzi wa madarasa Wilaya ya Bunda ilipata Bilioni 3.6 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa katika Halmashauri zake zote mbili.

“Kwa sasa Wilaya ya Bunda inamadarasa ya kutosha kwa shule za sekondari na katika baadhi ya maeneo kuna ziada ya vyumba vya madarasa” amesema Mheshimiwa Nassari.

Shule za msingi na sekondari zilifunguliwa tarehe 9 Januari, 2022 hapa nchini na hadi sasa usajiri wa wanafunzi wapya unaendelea katika shule zote hapa nchini.

Katika ziara hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Mara aliambatana na Mkuu wa Wilaya ya Bunda, watumishi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, maafisa kutoka ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bunda, viongozi na maafisa wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda.  

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa