• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RAS Kusaya awataka wananchi kutumia huduma za benki

Posted on: December 19th, 2024

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Gerald Musabila Kusaya leo amezindua rasmi Tawi la Benki ya CRDB katika eneo la Mugango na kuwataka wananchi wa Wilaya ya Musoma kutumia huduma za benki katika kutunza fedha na kuendesha biashara zao.

Akizungumza katika hafla ya ufunguzi wa tawi hilo, Bwana Kusaya amesema kuna faida nyingi kwa wananchi kutunza fedha zao benki ikiwa ni pamoja na usalama wa fedha dhidi ya majanga, wizi, urahisi wa kupata mikopo ya biashara na urahisi wa kufanya malipo kutumia mifumo ya kidijiti ya benki.

“Mtu akitumia benki itakuwa ni rahisi kwa benki inayotaka kumpatia mkopo wa biashara kufuatilia rekodi za mapato na matumizi katika biashara hiyo ili kumwezesha kupata mkopo kama atahitaji” amesema Bwana Kusaya.

Bwana Kusaya ameipongeza Benki ya CRDB kwa kazi kubwa wanayoifanya katika Sekta ya Fedha hapa nchini na kuitaka benki hiyo kutoa mikopo yenye masharti na riba nafuu kwa wananchi ili kuwahamasisha kuachana na mikopo inayotolewa na wafanyabiashara wanaotoza riba kubwa.

Aidha, Bwana Kusaya ameitaka Benki ya CRDB kuendelea kutoa elimu ya masuala ya fedha kwa umma na kuwahamasisha wananchi kutumia benki katika kuhifadhi fedha zao na kuendesha na kusimamia biashara zao.

Bwana Kusaya amewataka wananchi watakaopata mikopo ya biashara katika benki hiyo kurejesha mikopo mapema ili kuwajengea uaminifu katika Benki hiyo na benki nyingine na kuwawezesha kupata mikopo wakati mwingine ya kuendeleza biashara zao.

Kwa upande wake, Afisa Mkuu wa Biashara wa Benki ya CRDB, Bwana Boma Raballa amemshukuru Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara na wageni wote walioshiriki katika hafla ya uzinduzi wa Tawi la Mugango kwa kuweza kushiriki.

Bwana Raballa amesema kuwa Benki hiyo inayo matawi zaidi ya 250 na machine za kutolea fedha zaidi ya 550 pamoja na mawakala waliosambaa na kutoa huduma katika maeneo mbalimbali hapa nchini.

Bwana Raballa amemshukuru Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini Prof. Sospeter Muhongo kwa jitihada zake za ufuatiliaji na kuhakikisha Benki ya CRDB inafungua tawi katika eneo la Mugango akiamini wananchi wake hawawezi kuendelea bila ya kupata benki ya uhakika katika eneo hilo.

Bwana Raballa amewataka wakulima, wavuvi na wafugaji kuchangamkia akaunti mpya za kilimo za Benki ya CRDB ambazo hazina makato na kwa baadae zitawasaidia katika kupata mikopo inayotolewa na benki hiyo.  

Kwa upande wake, Meneja wa CRDB Kanda ya Ziwa Bwana Lusingi Sitta amesema kuwa kwa sasa baada ya kufungua Tawi la Mugango, Benki ya CRDB ina matawi tisa katika Mkoa wa Mara na tawi jingine la kumi linatarajiwa kufunguliwa katika Mkoa wa Mara karibuni.

Bwana Sitta amesema Tawi la Mugango linatarajiwa kutoa huduma zote za kibenki ikiwa ni pamoja na kufungua akaunti, kutoa mikopo, kutoa ushauri wa kibiashara kwa wafanyabiashara wadogo na kuwahudumia wateja wakubwa na wadogo wa benki hiyo.  

Bwana Sitta amewapongeza wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma kwa mwitikio mkubwa katika kuitumia benki hiyo na hususan wakulima, wavuvi na wafanyabiashara za samaki waliopo katika eneo hilo.

“Tangu Tawi la Mugango lilipoanza kufanyakazi Aprili, 2024 mpaka sasa tayari tumepata wateja zaidi ya 1000 waliofungua akaunti mpya za benki na wanaopata huduma katika tawi hili” amesema Bwana Sitta.

Bwana Sitta amewataka watumishi wa taasisi mbalimbali zilizopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Musoma kuitumia benki hiyo badala ya kusafiri umbali mrefu kufuata huduma za kibenki katika Manispaa ya Musoma.

Tawi la Mugango la Benki ya CRDB limeanza kutoa huduma kwa wananchi kuanzia mwezi Aprili, 2024 na linatoa huduma kwa taasisi mbalimbali za Serikali, binafsi na wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa