• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RAS awataka wasimamizi wa Elimu kuwajibika

Posted on: December 19th, 2023

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Msalika Robert Makungu leo amefungua mafunzo ya siku tatu kwa Walimu Wakuu 140 na Maafisa Elimu Kata 30 wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti na kuwataka wasimamizi wa elimu katika ngazi mbalimbali kutimiza wajibu wao.

Akizungumza katika ufunguzi wa mafunzo hayo, Bwana Makungu amewataka walimu kujitathmini ni vitu gani wanajivunia katika utumishi wao na kuwataka kusimamia maadili ya walimu na wanafunzi wanaowalea ili kujenga Taifa lenye maadili mazuri.

“Walimu Wakuu na Maafisa Elimu Kata  tukitimiza wajibu wetu vizuri kusimamia ufundishaji na ujifunzaji katika shule zetu, walimu watabadilika katika kufundisha wanafunzi na wanafunzi wataongeza juhudi kwa kuwa wanafuatiliwa na walimu wao” amesema Bwana Makungu.

Bwana Makungu amewataka Walimu Wakuu na Maafisa Elimu Kata kuimarisha mawasiliano baina yao na wanaowaongoza na wasimamizi wa elimu katika ngazi za Halmashauri na Mikoa ili kusaidia kutatua changamoto zinazowakabili walimu.

Bwana Makungu ameeleza kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti haijafanya vizuri sana kwenye matokeo ya mtihani wa Darasa la Saba wa mwaka 2023 na mafunzo haya yawe chachu ya kuboresha ufaulu.

Bwana Makungu amewaacha Walimu Wakuu na Maafisa Elimu Kata kuacha kusimamia kwa mazoea bali wasimamie kwa kufuata sheria, taratibu na kanuni zinazosimamia Sekta ya Elimu hapa nchini.

“Mkisimamia kwa mazoea ndio mwanzo wa kutengeneza msingi wa hoja ya kuondolewa kwenye madaraka mliyonayo”amesema Bwana Makungu.

Bwana Makungu amewakumbusha umuhimu wa Walimu Wakuu kuwashirikisha wlaimu wote katika utendaji wao na kuancha kutengeneza makundi kati ya watumishi waliopo ili kuongeza ufanisi katika ufundishaji na ujifunzaji.

Kwa upande wake, Mratibu wa Mradi wa Shule Bora Bwana Samwel  Mwita ameeleza kuwa awali walibaini changamoto ya uongozi katika shule za msingi na Maafisa Elimu Kata na Wakala wa Maendeleo ya Elimu (ADEM) walikubali kutoa mafunzo ya uongozi katika ngazi hizo.

“Imebainika kuwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti kuna changamoto nyingi za kiuongozi kuliko Halmashauri nyingine za Mkoa wa Mara na ninaamini baada ya mafunzo haya Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti itabadilika kwa maana ya uongozi na usimamizi wa elimu” amesema Bwana Mwita.

Aidha, Bwana Mwita amewakaribisha wakufunzi kutoka Adem Mbeya, Bagamoyo na Mwanza na maafisa kutoka Benki ya Dunia ambao wamekuja kuangalia namna mafunzo yanavyoweza kuleta matokeo chanya kwa viongozi. 

Bwana Mwita ameeleza kuwa mwaka huu, Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti tu ndio itakayopatiwa mafunzo hayo, lakini Halmashauri nyingine za Mkoa wa Mara zitapatiwa mafunzo kama hayo mwakani.

Akitoa neno la shukrani Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Kambarage B, Mwal. Maswi Chacha ameishukuru Serikali na Mradi wa Shule Bora kwa kuandaa mafunzo hayo kwa Walimu na Maafisa Elimu Kata na kuahidi kuyafanyia kazi maelekezo yote yaliyotolewa.

“Kwa niaba ya walimu wenzangu, ninaahidi tutashiriki kikamilifu katika mafunzo haya na kuyafanyia kazi maelekezo yote yaliyotolewa na viongozi na wakufunzi” amesema Bwana Chacha.

Bwana Chacha ameahidi watajitahidi kusimamia ufundishaji na ujifunzaji ili matokeo ya mitihani inayokuja iwe na mabadiliko chanya.

 Ufunguzi wa mafunzo hayo umehudhuriwa pia na baadhi ya Maafisa kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara na Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Mwenge wa Uhuru Wapitisha miradi 68 ya bilioni 26.5 Mara

    August 23, 2025
  • RC Mtambi akutana na viongozi wa dini na kuwasistiza kuhamasisha amani

    August 22, 2025
  • Wananchi Rorya wahimizwa kutumia nishati safi ya kupikia

    August 19, 2025
  • Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa awasha Mwenge wa Mwitongo kwa mara ya 61

    August 18, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa