• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RAS aongoza makabidhiano ya magari yaliyotolewa na Amref

Posted on: March 5th, 2025

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara leo tarehe 05 Machi, 2025 ameongoza hafla ya kukabidhi magari matatu yaliyotolewa na Shirika llisilo la kiserikali la Amref kwa ajili ya kusaidia shughuli za usimamizi wa sekta ya afya katika Mkoa wa Mara.

Akizungumza katika hafla ya kukabidhi magari hayo, Bwana kusaya amewataka maafisa wanaokabidhiwa magari hayo kuyatumia vizuri kwenye shughuli za usimamizi wa sekta ya afya zilizokusudiwa na Shirika la Amref.

“Mimi nitafuatilia kwa karibu matumizi ya magari haya ili yatumike kwa makusudio yaliyopangwa ikiwa ni pamoja na kufuatilia muda wa matengenezo” amesema Bwana Kusaya.

Bwana Kusaya amelishukuru Shirika la Amref kwa kutoa msaada wa magari hayo na ni nyenzo muhimu katika utoaji wa huduma bora za afya kwa wananchi wa Mkoa wa Mara na kuahidi kuwa magari haya tutayatunza ili yaendelee kutoa huduma.

Kwa upande wake, Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Afya Dkt. Zabroni Masatu amesema kuwa magari yaliyopokelewa ni Nissan Patrol moja kwa ajili ya matumizi ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara na magari mawili Toyota hardtop ambayo yamekabidhiwa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma na Halmashauri ya Mji wa Bunda.

Dkt. Masatu amelishukuru Shirika la Amref kwa msaada huo na kusema kuwa mahitaji ya magari ya usimamizi wa shughuli mbalimbali ya sekta za afya ikiwa ni pamoja na ukaguzi wa miradi ya sekta hiyo na vituo vya kutolea huduma za afya.

Kwa upande wake, Meneja wa Mradi wa Mkoa wa Mara Dkt. Revocatus Masanja amesema Amref imetoa magari matatu yaliyokuwa yanatumika kwa ajili ya usimamizi wa mradi wa ukimwi katika Mkoa wa Mara kwa ajili ya Halmashauri na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara kutokana na shirika hilo kuona mahitaji.

“Magari haya bado ni mazima yakitumika vizuri yatasaidia kutatua uhaba wa changamoto za magari kwa ajili ya usimamizi wa vituo vya kutolea huduma za afya na miradi ya sekta ya afya” amesema Dkt. Masanja.

Dkt. Masanja ameishukuru Serikali ya Mkoa wa Mara kwa ushirikiano mkubwa ambao umekuwa ukitoa kwa wadau mbalimbali ikiwemo Shirika la Amref na kuupongeza Mkoa kwa kujali afya za wananchi wake.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma Bwana Msongera Palera amelishukuru Shirika la Amref kwa kutoa msaada huo ambao utatatua upunguvu mkubwa wa magari katika Halmashauri hiyo.

“Awali tulikuwa tunaazima magari Amref mara kwa mara na sasa wameona watupatie gari moja iwe ya kwetu ili tuweze kuwahudumia wananchi vizuri zaidi” amesema Bwana Palera.

Bwana Palera amesema Halmashauri yao ina eneo kubwa sana na inavituo vingi vya kutolea huduma za afya kwenye vimesambaa maeneo mbalimbali ya Halmashauri hiyo na inakuwa vigumu kwa wasimamizi wa sekta ya afya kama hawana usafiri wa uhakika.

Hafla ya mapokezi ya magari hayo imehudhuriwa na baadhi ya watumishi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, wenyeviti wa Halmashauri, Wakurugenzi wa Halmashauri, Wakuu wa Divisheni za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe wa Halmashauri hizo.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa