• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Polisi yakamata magunia 67ya bangi

Posted on: August 18th, 2022

Polisi Kanda Maalum ya Tarime/ Rorya imekamata magunia 67 ya madawa ya kulevya aina ya bangi yenye uzito wa kilogramu 3,350 katika Kijiji cha Nyamwigura, Kata ya Binagi, Tarafa ya Inchage Wilaya ya Tarime tarehe 9 Agosti, 2022.

Akizungumza na Waandishi wa Habari, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Polisi wa Tarime/ Rorya, ACP Geofrey Sarakikya ameeleza kuwa bangi hiyo ilikuwa kwenye lori aina ya fuso yenye namba za usajiri T 597 CFY mali ya Bwana Festo Mmassy, Mkazi wa Arusha.

“Dereva wa gari hilo Bwana Samson Mollel alifanikiwa kutoroka kabla ya kukamatwa na kuwaacha wenzake wawili ndani ya gari hilo ambao walikamatwa na msako mkali unaendelea kuwatafuta wahusika wengine wa kosa hilo” alisema Bwana Sarakikya.

Bwana Sarakikya ameeleza kuwa wahalifu hao waliyaficha magunia hayo ndani ya gari kwa kuyafunika na mikungu ya ndizi mbichi ili yasiweze kuonekana wakati wa ukaguzi na uchunguzi wa awali umebaini kuwa bangi hiyo ilikuwa inasafirishwa kwenda Dar es Salaam.

Kamanda huyo wa Polisi wa Mkoa wa Kipolisi wa Tarime/ Rorya ameeleza kuwa watuhumiwa wawili waliokamatwa watafikishwa mahakamani pindi upelelezi utakapokamilika.

Wakati huo huo, siku hiyo hiyo katika Kijiji cha Mpakani, Kata ya Sirari katika Wilaya ya Tarime Polisi imekamata mawe mawili yanayodhaniwa kuwa ni ya dhahabu yenye uzito unaokadiriwa kuwa gramu 200 yakiwa yanatoroshwa kwenda nchi Jirani ya Kenya.

Bwana Sarakikya ameeleza kuwa mawe hayo yalikuwa yamefichwa ndani ya gari namba aina ya Land Cruiser Prado, rangi nyeusi yenye namba za usajiri KDH 718 T inayomilikiwa na mtu anayesadikiwa ni Raia wa Kenya anayefahamika kwa jina moja la Matiko.

Kwa mujibu wa Bwana Sarakikya, tayari watuhumiwa wawili wameshakamatwa na wanaendelea kuhojiwa na watafikishwa mahakamani pindi upelelezi utakapokamilika.

Mkoa wa Kipolisi (Kanda Maalum ya) Tarime/ Rorya una jumla ya Wilaya za Kipolisi sita ambazo ni Tarime, Sirari, Nyamwaga, Kinesi, Shirati na Rorya.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa