• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Pinda awaongoza Watanzania Miaka 100 ya Mwalimu Nyerere

Posted on: April 14th, 2022

Waziri Mkuu Mstaafu Mheshimiwa Mizengo Kayanza Pinda leo amewaongoza watanzania katika kumbukumbu ya miaka 100 ya tangu kuzaliwa kwa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere iliyofanyika katika Uwanja wa Mwenge, wilayani Butiama.

Mheshimiwa Pinda ambaye amemwakilisha Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Majaliwa Kassim Majaliwa katika maadhimisho hayo amewataka watanzania kuendelea kumuenzi Mwalimu Nyerere kwa vitendo.

“Mwalimu Nyerere kama walivyo Marais wengine wote wa Tanzania alifanya mambo mengi sana mazuri na yenye manufaa kwa Taifa letu, hivyo nitoe wito kwenu tuendelee kumuenzi” alisema Mheshimiwa Pinda.

Mheshimiwa Pinda amewataka Watanzania kufanyakazi kwa bidii na kufuata misingi aliyoiacha ikiwemo amani, umoja, upendo, mshikamano, uadilifu na uzalendo kwa Taifa.

Kwa upande wake, Chifu wa Kabila la Wazanaki na Kiongozi wa Familia ya Mwalimu Nyerere, Chifu Japhet Wanzagi ameiomba Serikali kukamilisha uanzishwaji wa Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere kinachoanzishwa katika Wilaya ya Butiama.

“Sisi kama familia tunatamani sana, Mama Maria Nyerere naye anatamani kuona wanafunzi wa Chuo hiki wawe wameanza kusoma hapo kabla yeye hajafa” alisema Chifu Wanzagi.

Chifu Wanzagi ameeleza kuwa familia ya Mwalimu Nyerere inaridhika na jinsi Tanzania na dunia kwa ujumla inavyomkumbuka na kumuenzi Mwalimu Julius Kambarage Nyerere hata baada ya kifo chake.

Chifu Wanzagi ameiomba Serikali kujenga barabara ya kwenda kwenye mashamba ya Mwalimu Nyerere ili vijana na watanzania ambao wangependa kujifunza maisha ya Mwalimu Nyerere waweze kuyatembelea mashamba bila usumbufu.

Wakati huo huo, Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi ameishukuru Serikali kwa kuanzisha maadhimisho hay ana kukubali yafanyike katika Mkoa wa Mara.

Aidha Mheshimiwa Hapi ameishukuru sana Serikali ya Awamu ya sita kwa kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo katika Mkoa wa Mara.

“Kwa sasa hivi tunatarajia mambo yakienda vizuri, Uwanja wa Ndege wa Musoma utaanza kutumika kuanzia Desemba, 2022 na ndege za Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) zitaanza kutua tena Musoma kama ilivyokuwa awali” alisema Mheshimiwa Hapi.

Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa kuanza kutua kwa ndege hizo kutaongeza idadi ya wataalii katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na kuinua maendeleo kwa wananchi wa Mkoa wa Mara na mikoa ya Jirani.

Mwalimu Nyerere alizaliwa tarehe 13 Aprili, 1922 katika Kijiji cha Butiama katika iliyokuwa Wilaya ya Musoma kwa wakati huo ambapo kwa sasa ni Wilaya ya Butiama.  

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa