• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Nchimbi atoa maelekezo Changamoto ya Umeme Kwangwa

Posted on: April 23rd, 2025

Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi leo tarehe 23 Aprili, 2025 ametembelea na kukagua Uwanja wa Ndege Musoma na ujenzi katika Hospitali ya Rufaa ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere (Kwangwa) na kutoa wiki mbili kwa Wizara ya Fedha kuilipa TEMESA madai yake ili kutatua changamoto ya umeme katika Hospitali ya Kwangwa.

Mhe. Nchimbi ametoa maagizo hayo baada ya kupokea taarifa kuhusiana na madai ya Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) ambao umepata zabuni ya kutengeneza mfumo wa umeme na jenerata kwa ajili ya Hospitali hiyo hajalipwa kwa muda mrefu na kukwamisha utoaji wa huduma katika hospitali hiyo.

“Ninamwagiza Waziri wa Fedha alipe deni hilo ndani ya wiki mbili ili TEMESA wakamilishe kazi yao na umeme wa kutosha uweze kupatikana katika hospitali hii. Baada ya wiki mbili nitakupigia simu Mkuu wa Mkoa kujua kama fedha hizo zimeshaingia” amesema

Mhe. Nchimbi ameahidi kuendelea kufuatilia utekelezaji na ukamilishaji wa miradi ya kimkakati katika Mkoa wa Mara na kuipongeza Wizara ya Afya na Mkoa wa Mara kwa utekelezaji wa mradi wa hospitali hiyo na usimamizi mzuri katika utoaji wa huduma kwa wananchi.

Mhe. Dkt. Nchimbi ameipongeza Mamlaka ya Viwanja vya Ndege (TAA) kwa upanuzi wa uwanja huo wenye historia kubwa katika maendeleo ya Tanzania na kuitaka Wizara ya Fedha kulipa shilingi bilioni 2.5 anazodai mkandarasi wa uwanja huo ili uanze kutumika kuanzia Septemba, 2025.

Mhe. Nchi ameitaka TAA na Wizara ya Fedha kuona namna mchakato wa ujenzi wa jengo la abiria utakavyoweza kuharakishwa ili kupata jengo la kisasa la abiria katika Uwanja wa Ndege Musoma.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Afya Mhe. Dkt. Godwin Mollel amesema baada ya hospitali hiyo kuanza kufanya kazi imepunguza asilimia 70 ya rufaa kutoka Mkoa wa Mara kwenda Hospitali ya Rufaa ya Kanda Bugando jambo ambalo limesaidia kuokoa maisha ya wananchi.

Mhe. Mollel amesema Hospitali hiyo tangu imeanza kufanya kazi inatoa huduma nzuri kwa wagonjwa na kupunguza rufaa za wagonjwa kwenda nje ya Mkoa wa Mara kwa matibabu ya kibingwa kwa kuwa sasa yanapatikana Musoma.

Dkt. Mollel amesema Wizara ya Afya inalifanyia kazi ombi la kutoa eneo la Hospitali hiyo kwa ajili ya ujenzi wa Chuo Kikuu cha Tiba ili kuimarisha zaidi huduma za afya katika Mkoa wa Mara.

Awali, akitoa taarifa za mradi wa Hospitali ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo Dkt. Osmund Dyegula amesema Hospitali hiyo inahudumia wagonjwa wengi kutoka nchi jirani na kwa mwaka huu pekee imehudumia wagonjwa 161 kutoka nchi za Kenya na Uganda.

Dkt. Dyegula amesema changamoto ya umeme ikitatuliwa itaiwezesha Hospitali hiyo kuhudumia wagonjwa wengi zaidi kutoka Mkoa wa Mara, Simiyu na nchi jirani na hususan wanaosumbuliwa na matatizo ya figo na waliopata ajali.

Akitoa taarifa ya ujenzi wa uwanja wa ndege, Meneja wa TANROADS Mkoa wa Mara Mhandisi Vedastus Maribe amesema uwanja huo utakapokamilika utawezesha ndege kubwa za abiria kuweza kutua na kuruka.

Mhandisi Maribe amesema tayari serikali imeshalipa fidia kwa awamu mbili jumla ya bilioni nane na wananchi 144 wamelipwa na kwa awamu ya tatu inahusisha wananchi 58 na gharama ya shilingi bilioni 5.2 kwa ajili ya eneo la kujenga jengo la abiria.

Mhandisi Maribe amesema ujenzi wa uwanja huo umetoa ajira kwa wataalamu mbalimbali 116 na kati yao wazawa 113 huku kukiwa na wataalamu watatu kutoka nje ya nchi.

Mhandisi Maribe anasema uwanja huo umechelewa kukamilika kutokana na ucheleweshwaji ya malipo ya mkandarasi lakini kwa sasa upo katika hatua nzuri. 

Akizungumza katika ziara hiyo, Mbunge wa Musoma Mjini Mhe. Vedastus Mathayo amesema Hospitali hiyo inachangamoto kubwa ya umeme jambo ambalo linazuia kutumia vifaa mbalimbali vilivyonunuliwa kwa ajili ya kuwahudumia wagonjwa.

Mhe. Mathayo amemuomba Mhe. Nchimbi kufuatilia madai ya shilingi bilioni 1.5 yaliyowasilishwa na TEMESA tangu Desemba, 2025 ambayo hadi sasa hazijalipwa na mradi huo umesimama huku wananchi wakishindwa kupata huduma stahiki katika hospitali hiyo.

Aidha, Mhe. Mathayo amemuomba Mhe. Dkt. Nchimbi kufuatilia uanzishwaji wa Kampasi ya Chuo Kikuu cha Mwalimu Nyerere cha Kilimo na Teknolojia (MJUNUAT) Butiama katika eneo la Hospitali hiyo ambapo tayari ekari 20 zimetengwa katika hospitali hiyo kwa ajili ya chuo hicho.

Kwa upande wake, Mbunge wa Musoma Vijijini Prof. Sospiter Muhongo amesema ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere uliasisiwa na viongozi wa TANU miaka ya 1975 wakiwa na lengo la kujenga Hospitali ya Rufaa ya Kanda.

Prof. Muhongo amesema mradi huo baadaye ulipelekwa Serikalini na kwa sasa unatoa huduma nzuri kwa wananchi na ukikamilika mapema utaokoa maisha ya wananchi wa Mkoa wa Mara na maeneo jirani.

Amemuomba Mhe. Nchimbi kufuatilia suala la kuanzishwa kwa Chuo Kikuu cha Tiba katika eneo hilo ambalo amesema limechukua muda mrefu kuanza kutekelezwa.

Katika ziara hiyo, Mhe. Nchimbi ameambatana na viongozi na Watendaji wa CCM na Serikali na kauli mbiu ya miaka 61 ya Muungano ni “Muungano wetu ni Dhamana, heshima na tunu ya Taifa, Shiriki Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025”.  

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa