• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Naibu Waziri Mkuu aongoza Mazishi ya Jenerali Musuguri

Posted on: November 4th, 2024

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Doto Mashaka Biteko leo amewaongoza mamia ya waombolezaji katika mazishi ya aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri yaliyofanyika nyumbani kwake katika Kijiji cha Butiama, Wilaya ya Butiama, Mkoa wa Mara.

Akitoa salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Mhe. Dkt. Biteko amesema Jenerali Musuguri ametoa sehemu kubwa ya maisha yake kuhakikisha Tanzania inakuwa na amani, usalama na mshikamano wa kitaifa na kuwataka watu wote kuiga mfano wake na kujiuliza ni jambo gani wao kama wananchi wa Tanzania watakumbukwa nalo.

“Katika uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo? Huyu ameacha alama ya uzalendo, kujitoa kwake kuipenda nchi---- alikuwa mstari wa mbele kuliokoa taifa lake, tujiulize sisi tuliobakia tutaacha alama gani” amesema Mhe. Dkt. Biteko.

Mhe. Dkt. Biteko amewataka Watanzania kumuenzi Jenerali Musuguri kwa kuilinda amani na utulivu wa Nchi yetu na hasa katika kipindi hiki nchi inapoelekea katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa na Uchaguzi Mkuu mwaka 2025 na kuongeza kuwa bila amani na utulivu hamna maendeleo yanayoweza kupatikana.

Dkt. Biteko amesema Jenerali Musuguri wakati wote akiwa Jeshini alikuwa mstari wa mbele katika kuliokoa Taifa na kuongeza kuwa Serikali daima itauenzi mchango wake mkubwa alioutoa wakati wa uhai wake kwa kuendelea kuhakikisha kuwa Tanzania inakuwa na amani na utulivu.  

Akizungumza kwa niaba ya wazee wa Kizanaki, Chifu wa Kabila la Wazanaki, na Kiongozi wa familia ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Chifu Japhet Wanzagi amesema wananchi wa Butiama na Watanzania tumeondokewa na mtu muhimu sana aliyekuwa na karama, uwezo na kipaji cha ajabu na kumwelezea marehemu Musuguri kuwa alikuwa mpenda watu, mnyenyekevu aliyemjali na kumthamini kila mtu.

“Huyu hakuwa na ukwasi wa mali bali tajiri wa utu wema, watu wengi tulipenda kukaa nae na kuzungumza nae mara kwa mara, alikuwa ni mkarimu na mwenye moyo wa kuwasaidia wahitaji na kuzivaa shida zao” amesema Chifu Wanzagi.

Chifu Wanzagi amesema marehemu alikuwa anauwezo wa kuongea lugha nyingi za makabila ya Afrika Mashariki na hivyo watu wengi walipenda kumsikiliza akiongea kwa kuwa alikuwa anazifahamu na kuziongea lugha zao.

Kwa upande wake, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob Mkunda amesema kifo cha Jenerali Musuguri ni msiba mkubwa kwa Tanzania na Jeshi la Wananchi wa Tanzania litaendelea kuuenzi mchango wake katika kuanzishwa kwa jeshi hilo na mazuri yote aliyofanyanya wakati alipolitumikia jeshi hilo kwa zaidi ya miaka 45.

“Alishiriki vita vya Pili vya Dunia ambavyo vilimjenga, kumkomaza  na kumpa uzoefu mkubwa na aliporejea nchini aliutumia uzoefu huo kwa ajili ya kujenga nchi yake na kuandaa mipango mbalimbali ya kivita ambayo nchi yetu ilishiriki ikiwemo Vita vya Kagera na vita vya ukombozi wa nchi za Kusini mwa Bara la Afrika” amesema Jenerali Mkunda.

Jenerali Mkunda amesema Tanzania itaendelea kumkumbuka kwa mchango wake mkubwa alioutoa katika Vita vya Kagera na pamoja na shughuli mbalimbali za kijeshi zilizofanyika hapa nchini na nje ya Nchi ya Tanzania kwa nyakati tofauti tofauti.

Jenerali Mkunda amemtaja Jenerali Musuguri kuwa wakati wa uhai wake na hususan akiwa jeshini alikuwa shupavu, hodari, shujaa na Jenerali aliyewapenda sana askari wake.  

Akitoa mahubiri wakati wa misa ya mazishi, Askofu wa Jimbo Katoliki la Musoma Michael Msonganzila amesema marehemu Musuguri katika uhai wake alikuwa anawaunganisha watu wa makundi yote na  ndio sababu ya watu wengi kujitokeza kwa ajili ya kumuaga na kumsindikiza katika mazishi yake.  

Mhashamu Askofu Msonganzila amesema Mungu aliwaumba binadamu ili wamjue, wampende, wamtumikie na mwisho waende kwake mbinguni na hivyo Jenerali Musuguri yeye ameianza hiyo safari ya kwenda mbinguni akiwa ameacha alama kubwa hapa duniani.

Askofu Msonganzila amewataka waombolezaji kuendelea kumuombea Jenerali Musuguri na kujiombea wao wenyewe kwa kuwa kwa mujibu wa imani, Yesu alikufa, akazikwa na akafufuka na Mungu atawakutanisha wote waliofariki wakimwamini na Yesu Kristu.  

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Dkt. Stergomena Lawrence Tax, Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi, Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini, Kamati ya Usalama ya Mkoa wa Mara na baadhi ya Wakuu wa Wilaya za Mkoa wa Mara, viongozi wa Chama cha Mapinduzi na viongozi wa taasisi za umma na binafsi.

Viongozi wengine waliohudhuria mazishi hayo ni Wakuu wa Jeshi la Ulinzi Wastaafu, Katibu Mkuu Kiongozi Mstaafu Ndugu Philemon Luhanjo, Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhe. Charles Makongoro Nyerere, wakuu wa vyombo vya ulinzi wastaafu na baadhi ya maafisa na watumishi wa umma wa Mkoa wa Mara wameshiriki mazishi hayo.

Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alizaliwa tarehe 4 Januari, 1920 katika Kijiji cha Butiama na kufariki tarehe 29 Oktoba, 2024 katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando iliyopo Mwanza na leo amezikwa kwa heshima za kijeshi na kupigiwa mizinga ya heshima 17 katika Kijiji cha Butiama, Wilaya ya Butiama Mkoa wa Mara.  

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa