• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mzee awataka walimu kuwa wabunifu

Posted on: January 6th, 2023

MZEE AWATAKA WALIMU KUWA WABUNIFU

Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Suleiman Mungiya Mzee leo amewataka walimu wa shule mbalimbali katika Mkoa wa Mara kuwa wabunifu na kujiongeza katika utekelezaji wa majukumu yao.

Mheshimiwa Mzee ametoa wito huo wakati akifanya ziara ya kupokea vyumba vya madarasa katika Wilaya ya Serengeti na kuwaelekeza walimu kuanzisha miradi mbalimbali ya kuongeza mapato ya shule ili kuweza kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili.

“Walimu wetu hawana ubunifu, wa kujiongezea au kufanya mabadiliko katika shule zetu, Shule zinaweza kufanya biashara ndogo ndogo na kupata pesa za kuweza kutatua changamoto ndogo ndogo zinazowakabili” alisema Mheshimiwa Mzee.

Mheshimiwa Mzee ameeleza kuwa miradi itakayoanzishwa inaweza kutoa huduma na elimu kwa vitendo kwa walimu na wanafunzi wanaosoma katika shule hizo na wananchi wanaowazunguka maeneo ya shule.  

Aidha, amewataka walimu kutumia fursa ya kuwa na wanafunzi wengi kubuni miradi ambayo itawasaidia kupata fedha za kutatua changamoto mbalimbali pindi zinapojitokeza.

Wakati huo huo, Mkuu wa Mkoa amewataka walimu na wasimamizi wa elimu kusimamia suala la uboreshaji wa mazingira ya shule kwa kupanda miti, maua, matunda na kuyasawazisha maeneo ya shule na kuzuia mmomonyoko wa udongo katika shule zao ili wanafunzi waweze kupita vizuri.

“Mazingira yanatakiwa yawe mazuri ili wanafunzi wapende kwenda shule na wakienda wajifunze kitu kutokana na ubunifu katika kuongeza mapato na kutunza mazingira” alisema Mheshimiwa Mzee.   

Katika ziara hiyo, kati ya shule tano alizotembelea, Shule ya Sekondari Rigicha pekee ilitoa taarifa ya kuwa na mradi wa shule wa ufugaji wa nyuki, lakini shule nyingine zilitoa taarifa ya kuwa na mpango wa kuanzisha miradi lakini bado hawajapata mtaji wa biashara.

Katika ziara hiyo, Mkuu wa Mkoa aliambatana na Mkuu wa Wilaya ya Serengeti, Katibu Tawala sehemu ya Elimu, Katibu Tawala sehemu ya Miundombinu, Kamati ya Usalama ya Wilaya ya Serengeti, watumishi ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, Menejimenti ya Wilaya ya Serengeti na viongozi wa CCM Wilaya ya Serengeti.  

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa