• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mwenge wa Uhuru wawasha Mwenge wa Mwitongo Butiama

Posted on: June 26th, 2021

Mwenge wa Uhuru unaoendelea na mbio zake katika Mkoa wa Mara umefika nyumbani kwa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na kuwasha mwenge wa asili unaofahamika kama Mwenge wa Mwitongo.

Mwenge wa Mwitongo umewashwa leo tarehe 26 Juni 2021 ikiwa ni sehemu ya Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa ambapo kila mwaka Mwenge wa Uhuru hupita nyumbani kwa Baba wa Taifa na kuwasha Mwenge wa Mwitongo kama kumbukumbu ya muasisi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa.

“Mwenge huu umekuwa ukiwashwa miaka yote tangu Baba wa Taifa akiwa hai kila Mwenge wa Uhuru unapofika katika Mkoa wa Mara, ni tukio zuri kwa kweli kulishuhudia” alisema mwananchi baada ya kuwashwa kwa mwenge huo.

Baada ya kuwasha Mwenge wa Mwitongo, viongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa walipata nafasi ya kusalimiana na familia ya Nyerere iliyoongozwa na Chifu Japhet Wanzagi Nyerere akiambatana na Mtoto wa Baba wa Taifa Bwana Madaraka Nyerere na wanafamilia wengine.

Aidha viongozi hao walitumia fursa hiyo kuzuru kaburi la Mwalimu Nyerere na wakiwa hapo waliweka mashada ya maua na kuwasha mishumaa.

Akiwa nyumbani kwa Baba wa Taifa pia, kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa alikabidhi pikipiki kwa kikundi cha vijana, kukagua mradi wa kikundi cha wanawake, kufungua kikundi cha wapinga rushwa na kupatiwa maelezo kuhusu Jukwaa la Mobile Kilimo.  

Aidha Kiongozi wa Mbio Maalum za Mwenge wa Uhuru kitaifa akiwa eneo hilo alitoa elimu kwa wananchi kuhusiana na ujumbe wa Mwenge kitaifa kwa mwaka 2021.

Mwenge wa Uhuru unakesha leo katika viwanja vya Shule ya Msingi Nyamsisi na kesho unatarajiwa kukabidhiwa katika Wilaya ya Bunda ili kukamilisha mbio zake katika Mkoa wa Mara.

 Mwenge wa Uhuru unatarajiwa kukabidhiwa katika Mkoa wa Simiyu tarehe 28 Juni 2021 asubuhi kuendelea na mbio zake mkoani humo.   

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa