• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mwenge wa Uhuru wapokelewa Mara

Posted on: July 4th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Said Mohamed Mtanda leo amepokea Mwenge wa Uhuru kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe.John Mongela katika viwanja vya Shule ya Msingi Robanda, Wilaya ya Serengeti.

Akizungumza wakati wa mapokezi ya Mwenge wa Uhuru Mhe. Mtanda ameeleza kuwa Mkoa wa Mara umejiandaa vizuri kukimbiza Mwenge wa Uhuru katika Halmashauri zake tisa ambazo ni Serengeti DC, Butiama DC, Tarime DC, Tarime TC, Rorya DC, Musoma MC, Musoma DC, Bunda TC na Bunda DC na kuukabidhi Mwenge wa Uhuru salama katika Mkoa wa Mwanza tarehe 13 Julai, 2023.

Mhe. Mtanda ameeleza kuwa kama ilivyo kawaida ya miaka yote Mwenge wa Uhuru ukiwa katika Mkoa wa Mara utawasha Mwenge wa Mwitongo nyumbani kwa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere katika Wilaya ya Butiama.

“Hili ni tukio kubwa na la kihistoria katika Mkoa wetu na ninawakaribisha sana kutembelea na kuweka mashada ya maua katika Kaburi na Kutembelea makumbusho ya Baba wa Taifa mkiwa katika Wilaya ya Butiama” amesema Mhe. Mtanda.

Wakati huo huo, Mhe. Mtanda ameeleza kuwa Mwenge wa Uhuru ukiwa katika Mkoa wa Mara utakimbizwa katika jumla ya kilomita 1097 na utapita katika miradi ya maendeleo 63 yenye thamani ya shilingi bilioni 17.

“Miradi inayopitiwa na Mwenge wa Uhuru ipo katika sekta za elimu, kilimo, ujenzi, maji, afya, mifugo, ustawi wa jamii, viwanda na biashara” ameeleza Mhe. Mtanda na kufafanua kuwa miradi hiyo imegharimiwa namichango ya wananchi wa Mkoa wa Mara, Halmashauri, Serikali Kuu na wahisani wa maendeleo.

Aidha, Mhe. Mtanda amempongeza Mhe. Mongela kwa kuhitimisha mbio za Mwenge wa Uhuru salama na kuwatunza vizuri wakimbiza Mwenge wa Uhuru Kitaifa wakati wote walipokuwa katika Mkoa wa Arusha.

Mapokezi ya Mwenge wa Uhuru yamehudhuriwa na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Mara, Kamati ya Usalama ya Mkoa, wajumbe wa Kamati ya Siasa ya Mkoa, Wakuu wa Wilaya, Meya na Wenyeviti wa Halmashauri, Wakurugenzi wa Halmashauri, wakuu wa taasisi za umma na binafsi, viongozi wa vyama vya siasa na viongozi wa dini.

Wengine waliohudhuria ni Wakuu wa Idara na Vitengo kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, viongozi wa vyama vya wafanyakazi, viongozi wa mila, watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara na Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Demokrasia inaendelea kupevuka katika Mkoa wa Mara: Mtambi

    October 16, 2025
  • Biteko aitaka CWT kuendana na kasi ya mabadiliko duniani

    October 16, 2025
  • RC awapokea Maafisa na wanafunzi kutoka Chuo cha Jeshi cha CSC

    October 13, 2025
  • RC awapokea Madaktari Bingwa wa Mama Samia 64 Mara

    October 13, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa