• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtanda: Mgawanyo wa CSR ufuate Sheria

Posted on: October 24th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Said Mohamed Mtanda leo amezungumza na wananchi wa Kata ya Nyarukoba, Halmashauri ya Wilaya ya Tarime na kutaka fedha ya uwajibikaji kwa jamii (CSR) inayotolewa na Mgodi wa Dhahabu wa North Mara kugawanywa kwa mujibu wa Kanuni za Wajibu wa Wamiliki wa Leseni za Madini kwa Jamii za Mwaka 2023.

Akizungumza na wananchi hao katika uwanja wa Shule ya Sekondari Bwirege, Mheshimiwa Mtanda ameeleza kuwa Kanuni hizo zinazotokana na Sheria ya Madini zinatoa mgawanyo wa makusanyo ya CSR kwa vijiji na Halmashauri ambayo inachimbwa madini  na kuziwezesha Halmashauri nzima kunufaika kutokana na uwepo wa migodi katika maeneo yao.

“Kwa mujibu wa Kanuni hizo asilimia 40 ya mapato ya CSR yatatumika katika miradi ya kijiji au mtaa ambapo shughuli za madini zinafanyika na asilimia 60 kwa ajili ya miradi ya Halmashauri ambako shughuli za madini zinafanyika” amesema Mhe. Mtanda.

Mhe. Mtanda pia ameeleza kuwa kwa mujibu wa kanuni hizo, Kamati ya Wataalam inayoongozwa na Mkurugenzi wa Halmashauri kama Mwenyekiti na Katibu wake kuwa Afisa Mipango na wajumbe wengine ni Afisa wa Tume ya Madini, Wawakilishi wawili wa mmiliki wa leseni , Mhandisi, Wakili wa Serikali, Afisa Mazingira, Afisa Maendeleo na Afisa kutokakatika mradi mahususi unaotekelewa na mpango husika.

Kwa mujibu wa Mhe. Mtanda, utekelezaji wa Kanuni hizo katika Halmashauri ya Wilaya ya Tarime utasaidia katika kupeleka maendeleo kwa Halmashauri nzima ya Tarime tofauti na ilivyokuwa awali kabla ya kanuni hizo ambapo vijiji 11 tu vilivyokuwa vinauzunguka mgodi vilikuwa vinanufaika.

Wakati huo huo, Mheshimiwa Mtanda amewaahidi wachimbaji madini wanaouzunguka Mgodi wa North Mara kupata fursa ya kutumia mtambo wa uchorongaji madini kufanya utafiti katika maeneo yao na hivyo kuwezesha uwekezaji katika maeneo ambayo yana uwezekano wa kupata madini.

“Kwa kutumia mtambo huu, Serikali ya Mkoa itafanya utaratibu wa kuiwezesha North Mara kuwasaidia wachimbaji wadogo kwa kuwawezesha kupima maeneo yao na kuwawezesha kwa utaalamu na ujuzi ili wachimbaji wadogo waweze kunufaika na migodi waliyonayo” amesema Mhe. Mtanda.

Aidha, amewataka wananchi wanaoishi kuzunguka mgodi huo kuacha tabia ya uvamizi katika mgodi wa North Mara na kilimo cha bangi badala yake wajielekeze kwenye kutafuta fedha kwa kufanya shughuli halali.

Mhe. Mtanda ametumia fursa hiyo kuwaonya watu wanaofadhili uvamizi wa mgodi na kilimo cha bangi katika Wilaya ya Tarime kuacha mara moja na Serikali ya Mkoa imeshapata orodha ya wafadhili hao na mkakati wa kuwashughulikia unaandaliwa.

Kwa upande wake, Diwani wa Kata ya Nyarokoba Mhe. Juma Matiko amemshukuru Mkuu wa Mkoa kwa kufanya mkutano na wananchi wa Kata hiyo na kufuatilia upatikanaji wa umeme katika Kituo cha Afya Genkuru kilichopo katika  Kata hiyo.

Mhe. Matiko  ameushukuru Mgodi wa North Mara kwa kutoa ajira kwa vijana 40 kutoka katika Kata hiyo wanaolinda katika eneo la mgodi jambo ambalo limeongeza upatikanaji wa ajira kwa vijana.

 Katika ziara hiyo, Mkuu wa Mkoa aliambatana na Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Kamati ya Usalama ya Wilaya ya Tarime na watendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime wakiongozwa na Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa