• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtanda awataka wanawake kuchangamkia fursa

Posted on: March 8th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Said Mohamed Mtanda leo ameongoza maadhimisho ya siku ya  wanawake Duniani ambayo katika Mkoa wa Mara yamefanyika Nyamswa, Wilaya ya Bunda na kuwataka wanawake kuchangamkia fursa mbalimbali ili kujiendeleza kiuchumi.

Akizungumza katika maadhimisho hayo, Mhe. Mtanda amewataka kuchangamkia fursa za mikopo inayotolewa na Serikali, taasisi za kifedha na kuwahimiza kujitokeza kwa wingi kuwania nafasi mbalimbali za uongozi katika chaguzi zijazo.

 “Serikali inatambua umuhimu wa wanawake katika jamii na kutenga mikopo ya aina mbalimbali kwa ajili yao kupitia mikopo ya Halmashauri, mikopo ya Benki ya Maendeleo ya Kilimo (TADB) na fursa nyingine zilizopo ili waweze kukuza uchumi wao na wasiwe wategemezi katika jamii” amesema Mhe. Mtanda.

Mhe. Mtanda ameeleza kuwa mikopo ya Halmashauri iliyokuwa imesimamishwa itaanza kutolewa hivi karibuni baada ya Serikali kukamilisha utaratibu mpya wa utoaji wa mikopo hiyo na kuzitaka Halmashauri kuendelea kuhifadhi fedha kwa ajili ya mikopo hiyo.

Wakati huo huo, Mkuu wa Mkoa wa Mara amewataka wanawake kujitokeza kwa wingi kuwania nafasi mbalimbali za uongozi na kuwataka wamuunge mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika uchaguzi wa mwaka 2025.

Mhe. Mtanda amesema kwa maendeleo yaliyofikiwa katika Mkoa wa Mara chini ya uongozi wa Rais Samia atashangaa kama wanawake wa Mkoa wa Mara hawatamuunga mkono Rais Samia katika uchaguzi ujao ili aendelee kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.  

Mhe. Mtanda amesema kwa sasa Watanzania na hususan wananchi wa Mkoa wa Mara wameelimishwa kwa vitendo kutokana na mambo mengi yanayofanywa na viongozi wanawake na anaamini jinsia haitakuwa kikwazo tena katika chaguzi zijazo na kuwataka wanawake kujitokeza kugombea nafasi mbalimbali.

Mkuu wa Mkoa amevitaka vyama vya siasa kuwapitisha wanawake wengi zaidi katika nafasi mbalimbali watakazoomba ili kutoa kigezo cha jinsia ya mtu katika nafasi za uongozi na kuliwezesha taifa kupata viongozi wazuri watakaoleta maendeleo.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Mara Bibi Nancy Msafiri ameeleza kuwa maadhimisho haya yanatokana na wanawake kutambuliwa kama sehemu muhimu ya jamii kutokana na uhodari, kujituma na kuwa wabunifu katika mambo mbalimbali.

Bibi Msafiri ameeleza kuwa ameitaka jamii kuwekeza kwa watoto wakike ili kuharakisha maendeleo ya jamii na kutoka mfano wa utendaji wa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan na viongozi wengine wanawake waliopo hapa nchini.  

Bibi Msafiri amewataka wanawake wa Mkoa wa Mara kujitokeza kwa wingi kuwania nafasi mbalimbali za uongozi katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka huu na Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025.

Kwa upande wake, Afisa Maendeleo ya Jamii Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara Bibi Neema Ibamba ameeleza kuwa maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yameanza mwaka 1975 katika nchi mbalimbali duniani ikiwemo Tanzania.

Bibi Ibamba ameeleza kuwa kwa sasa maadhimisho haya yanafanyika katika mikoa yote kila mwaka na kitaifa yanafanyika kila baada ya miaka mitano; na katika Mkoa wa Mara maadhimisho haya yamekuwa yakizunguka katika wilaya mbalimbali ambapo mwaka huu yamefanyika katika wilaya ya Bunda.

Bibi Neema akitoa salamu za wanawake ameiomba Serikali ya Mkoa wa Mara kuunga mkono shughuli za wanawake ili waweze kujikwamua kiuchumi.

Maadhimisho ya siku ya wanawake yamehudhuriwa pia na Wakuu wa Wilaya za Bunda, Butiama, Katibu Tawala wa Wilaya ya Bunda, Meya wa Manispaa ya Musoma na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Butiama, madiwani, wawakilishi wa Wakurugenzi wa Halmashauri, watumishi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, Halmashauri na Taasisi za Serikali zilizopo Mkoa wa Mara.

Wengine waliohudhuria ni viongozi wa vyama vya siasa, taasisi na mashirika yasiyo ya kiserikali na wananchi wa eneo la Nyamswa, Wilaya ya Bunda na kauli mbiu ya maadhimisho haya mwaka huu ni “Wekeza kwa Wanawake kuharakisha Maendeleo ya Taifa na Ustawi wa Jamii”.  

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa