• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MTANDA ataka Mara kudhibiti Kipindupindu

Posted on: January 25th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Said Mohamed Mtanda amezitaka Halmashauri kuchukua hatua za  kudhibiti kuenea kwa ugonjwa wa kipindupindu ambao tayari umeathiri mikoa ya jirani inayouzunguka Mkoa wa Mara.

Mhe. Mtanda ametoa agizo hilo wakati wa kikao cha tathmini ya utendaji kazi Mkoa wa Mara kilichofanyika ukumbi wa Uwekezaji na kuhudhuriwa na viongozi wa Wilaya na Menejimenti za Halmashauri zote za Mkoa wa Mara.

“Tayari mikoa yote tunayopakana nayo imesharipoti kuwepo kwa ugonjwa huu, sisi tuchukue hatua mapema ili kudhibiti kusambaa kwa kipindupindu na hususan wakati huu wa mvua, na Halmashauri zitoe uzito kwenye jambo hili” amesema Mhe. Mtanda.

Amezitaka Halmashauri kuhuisha timu za muitikio wa dharura, kuandaa vituo vya matibabu na kuweka dawa na vifaa tiba kwa ajili ya matibabu ya wagonjwa na mahitaji mwengine na kuandaa mpango wa dharura wa kukabiliana na mlipuko wa ugongwa huo.

Mhe. Mtanda amezitaka Halmashauri kuendelea kutoa elimu ya afya kwa umma kuhusu usafi wa mazingira na matumizi ya vyoo na kufanya tathmini ya upatikanaji wa huduma za maji na usafi wa mazingira katika maeneo yote.

Mhe. Mtanda amezitaka Halmashauri kufanya ukaguzi wa usafi katika masoko, shule, kwenye minada, kaya na maeneo ya biashara ili kuzuia uwezekani wa kutokea mlipuko.

Mkuu wa Mkoa ametoa wito kwa wananchi kuzingatia usafi, kuchemsha maji yakunywa, kutumia vyoo bora, kuosha matunda na mbogamboga kwa maji safi na kufanya usafi wa mazingira katika maeneo yao.

Mhe. Mtanda amewataka Wakuu wa Wilaya na viongozi wa Halmashauri kusimamia zoezi la usafi wa mazingira kila Jumamosi ya Mwisho wa mwezi na kutoa taarifa ya utekelezaji wa zoezi hilo.

Akizungumza katika kikao hicho, Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii Dkt. Zabroni Masatu amesema kwa sasa Mkoa wa Mara hauna wagonjwa wa kipindupindu lakini kutokana na mwingiliano uliopo, hatua za kutosha zisipochukuliwa ugonjwa huu unaweza kuingia na kuenea ndani ya muda mfupi.

 Dkt. Masatu ameeleza kuwa ugonjwa huu unasababishwa na vimelea vya bakteria vinavyoitwa Vibrio Cholera na huambukisha kupitia kula chakula au kunywa maji yaliyochafuliwa na vimelea vya ugonjwa huo na dalili zake ni kuhara mfululizo, kutapika, ngozi kusinyaa na kuhema haraka haraka.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC awapokea Maafisa na wanafunzi kutoka Chuo cha Jeshi cha CSC

    October 13, 2025
  • RC awapokea Madaktari Bingwa wa Mama Samia 64 Mara

    October 13, 2025
  • Mtambi aipongeza CDEA kwa kuanzisha Redio Butiama FM

    October 03, 2025
  • Mtambi awataka wajasiriamali kuwa na nidhamu ya fedha

    October 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa