• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtanda ataka Mara iwe Kinara wa Matumizi ya GoTHOMIS

Posted on: February 15th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Said Mohamed Mtanda leo amefunga mafunzo ya mfumo wa GoTHOMIS iliyoboreshwa kwa Maafisa Tehama na Watumishi wa Sekta ya Afya na kuwataka kuhakikisha kuwa Mkoa wa Mara unaongoza katika matumizi ya mfumo huo.

Akizungumza katika hafla ya kufunga mafunzo hayo, Mhe. Mtanda amewataka watumishi hao kuhakikisha mfumo wa GotHOMIS ulioboreshwa unafungwa na kutumika katika vituo vyote vya kutolea huduma za afya katika Mkoa wa Mara kabla ya Desemba, 2024.

“Mimi ninataka Mkoa wa Mara uonyeshe mfano wa kuigwa katika matumizi ya mfumo wa GoTHOMIS ulioboreshwa ili mikoa mingine waje kujifunza Mkoa wa Mara, na hiyo inawezekana tukiamua” amesema Mhe. Mtanda.

Mhe. Mtanda amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri kuhakikisha vituo vya kutolea huduma za afya vina vifaa vya Tehama vinavyohitajika kuwezesha mfumo huo kufanya kazi kwa ufanisi.

Amewataka Waganga Wakuu wa Halmashauri kuhakikisha kuwa wanapanga ratiba za kufanya mafunzo na kufunga mfumo kwenye vituo vyote vya kutolea huduma katika Halmashauri zao.

Mhe. Mtanda pia amewataka watumishi wa umma kujiwekea malengo na kufanyakazi kwa bidii ili kuyatimiza malengo ya kiutumishi na mtu binafsi.

Kwa upande wake, Mtaalamu wa Tehama kutoka Ofisi ya Rais, TAMISEMI Bwana Mark Tanda ameeleza kuwa kwa sasa mfumo huu umeboreshwa na hauhitaji kufungwa mitambo ya Tehama katika kila kituo, badala yake vituo vitahitajika kuwa na vitendea kazi na mtandao tu kuweza kuutumia.

Bwana Tunda ambaye alikuwa ni mmoja kati ya wakufunzi wa mafunzo hayo ameeleza kuwa mfumo huu utarahisisha upatikanaji wa taarifa za afya kutoa ngazi ya kutolea huduma za afya pamoja na ukusanyaji wa mapato katika vituo vya afya.

“Mfumo huu utaiwezesha Serikali kufuatilia dawa tangu zinavyotoka Bohari ya Madawa (MSD), Mikoa, Wilaya hadi kwenye vituo vya kutolea huduma za afya” amesema Bwana Tanda.

Bwana Tanda ameeleza kuwa faida nyingine ya mfumo huu, utaviwezesha vituo vya kutolea huduma za afya kufanya shughuli zake bila kutumia karatasi (paperless) na huduma zote kutolewa kupitia mfumo ikiwa ni pamoja na rufaa ya mgonjwa kwenda kituo kikubwa cha kutolea huduma.

Mfumo wa Menejimenti ya Taarifa katika Vituo vya Kutolea Huduma za Afya (GoTHOMIS)  ni mfumo wa kukusanya mapato na taarifa katika vituo vya kutolea huduma za afya umeanza kutumika hapa nchini muda mrefu lakini kwa sasa umeboreshwa na kuhitaji mafunzo kwa watumiaji wake na hususan watumishi wa Sekta ya Afya na Maafisa Tehama.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa