• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtanda ataka maji Butiama tarehe 10 Machi, 2024

Posted on: February 18th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Said Mohamed Mtanda leo amefanya ziara katika Wilaya ya Butiama na  kuiagiza Mamlaka ya Maji Mgango- Kiabakari kuhakikisha maji katika mradi wa Maji wa Mgango-Kiabakari Butiama yanatwafikia wananchi kuanzia tarehe 10 Machi, 2024 kama walivyoahidi.

Mhe. Mtanda ametoa agizo hilo wakati akiendelea na ziara yake kukagua ujenzi wa ofisi za Mamlaka ya Maji Mgango Kiabakari katika eneo la Sabasaba, Wilaya ya Butiama na kuongeza wananchi wa Wilaya ya Butiama wamechoka taarifa nzuri, wanataka maji ya uhakika.

“Mimi na Wananchi wa Butiama tumechoka taarifa nzuri za maendeleo ya mradi, kwa sasa kinachohitajika ni maji safi na salama kutoka katika mradi huu uliotumia fedha nyingi kutekelezwa” amesema Mhe. Mtanda.

Aidha, Bwana Mtanda ameahidi kuzungumza na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) ili waweze kuleta vifaa vinavyohitajika kwa ajili ya mradi huo kuanza kufanyakazi mapema ili wananchi waweze kuepukana na adha ya kukosa maji safi na salama.

Katika ziara hiyo, Mkuu wa Mkoa amekagua ujenzi wa jengo la ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Butiama, ujenzi wa jengo la Uhamiaji Wilaya ya Butiama na ujenzi wa jengo la Polisi Wilaya ya Butiama na ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Butiama.

Akiwa katika miradi hiyo, Mhe. Mtanda amewataka wataalamu kutekeleza maagizo yanayotolewa na viongozi kwa wakati na kuacha tabia ya kuchelewesha utekelezaji wa miradi ya maendeleo bila ya sababu za msingi.

Mhe. Mtanda amehitimisha ziara yake kwa kuzungumza na wakazi wa Kijiji cha Kiabakari, Kata ya Kukilango na kumwagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Butiama kuweka miundombinu ya dampo na vyoo katika eneo hilo.

Awali, akitoa taarifa kwa Mkuu wa Mkoa, Mkurugenzi wa Mamlaka ya Mgango Kiabakari Mhandisi Cosmas Sanda ameeleza kuwa mradi huo unaotekelezwa kwa shilingi bilioni 70.5 kwa sasa umefikia asilimia 97 ya utekelezaji wake.

Mhandisi Sanda ameeleza kuwa kwa sasa majaribio ya mitambo ya kusukuma maji kutoka kwenye chanzo hadi kwenye matenki unasubiria TANESCO wakamilishe kufunga umeme na wameahidi kufunga na kuleta vifaa vilivyosalia ndani ya wiki moja kuanzia leo.

Bwana Sanda ameeleza kuwa kwa mpangokazi na mkakati uliopo, Mamlaka hiyoinategemea wananchi wa Wilaya za Musoma, Bunda na Butiama kuanza kupata maji mara baada ya TANESCO kukamilisha ufungaji wa umeme katika maeneo hayo.

 Katika mkutano huo, Mkuu wa Mkoa alipata fursa ya kusikiliza na kushughulikia kero na changamoto za wananchi wa eneo hilo na kuwapongeza wananchi kwa shughuli mbalimbali za kujiletea maendeleo.  

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa