• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtanda apongeza ubunifu wa Mwalimu Yusufu Pangoma

Posted on: November 9th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Said Mohamed Mtanda leo tarehe 31 Oktoba, 2023 ametembelea Shule ya Msingi Ikorongo iliyopo katika Wilaya ya Serengeti na kumpongeza Mwalimu Yusuf Pangoma kwa ubunifu wake katika ufundishaji.

Mhe. Mtanda amesema hayo baada yeye na watu alioambatana naye kwenye ziara yake kushuhudia mwalimu Pangoma akiwa darasani akiwafundisha wanafunzi wa darasa la kwanza wa shule hiyo.

“Awali nilimuona huyu Mwalimu akifundisha kwenye mitandao ya kijamii nikafurahishwa naye na nikamuomba aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Ally Salum Hapi aje kumtembelea” amesema Mtanda.

Mhe. Mtanda ameeleza kuwa aliendelea kuwasiliana na Mwalimu Pangoma na alipoteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mara akaamua kwenda kumtembelea ili kumtia moyo katika kazi nzuri anayoifanya katika shule hiyo.

Mhe. Mtanda alitoa zawadi ya shilingi 200,000 kwa Mwalimu Pangoma, shilingi 100,000 kwa ajili ya chai ya walimu wa shule hiyo na kuahidi mifuko 100 ya simenti kwa ajili ya kukarabati majengo ya shule hiyo.

Mhe. Mtanda pia ameahidi kuliomba Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) kutoa madawati kwa ajili ya kupunguza uhaba wa madawati katika shule hiyo baada ya kushuhudia wanafunzi wengi wakikaa kwenye dawati moja.

Mkuu wa Mkoa pia alimwagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti kukamilisha darasa moja lililojengwa kwa nguvu za wananchi na kukarabati madarasa ya shule hiyo ili kupunguza msongamano wa wanafunzi madarasani. 

Aidha, Mhe. Mtanda amewataka walimu wa hiyo na watumishi wote kwa ujumla kujiendeleza kimasomo na kuchapa kazi kwa bidii ili waweze kujijenga zaidi katika maisha yao bila kujali sehemu wanapofanyia kazi.

“Haya mazingira ya kijijini yanaweza kuwa fursa kubwa kwako kama ukiamua kuyakubali na kufanya kazi kwa bidii na kujishughulisha na kilimo au ufugaji jambo ambalo aliyepo mjini hawezi kulifanya” amesema  Mhe. Mtanda.

Mhe. Mtanda pia aliwapongeza walimu wa shule hiyo kwa ufaulu mzuri wa wanafunzi katika mitihani ya darasa la saba kwa miaka minne mfululizo na kuwataka waendelee na ufaulu huo.

Katika kuunga mkono juhudi za ukarabati wa shule hiyo, Mkuu wa Wilaya ya Serengeti Dkt. Vincent Mashinji aliahidi kutoa sementi mifuko 50 kwa ajili ya ukarabati wa shule hiyo.

Wakati huo huo, Mhe. Said Mtanda amewataka wazazi kufuatilia maendeleo ya watoto wao wanaosoma katika shule mbalimbali ili kuweza kubaini mahudhurio ya wanafunzi na kama kuna tatizo mapema waweze kurekebisha.

Akizungumza na wazazi waliohudhuria kikao katika Shule ya Sekondari ya Morotonga, Mhe. Mtanda amesema bila wazazi kutoa ushirikiano kwa walimu, walimu peke yao hawawezi kuhakikisha ufaulu wa wanafunzi.

Amewapongeza wazazi hao kwa kuhudhuria na kuwakemea wazazi ambao waliitwa na hawakuhudhuria kikao hicho.

Katika ziara hiyo, Mkuu wa Mkoa aliambatana na Mkuu wa Wilaya ya Serengeti, Kamati ya Usalama ya Wilaya ya Serengeti, viongozi, Mkurugenzi na watendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa