• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MTANDA akabidhi magari ya usimamizi wa sekta ya afya

Posted on: February 10th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Said Mohamed Mtanda leo amekabidhi magari matano ya usimamizi wa Sekta ya Afya na kuwataka viongozi na wasimamizi wa sekta ya afya kuhakikisha magari hayo yanatumika kwa malengo yaliyokusudiwa.

Akizungumza wakati wa kukabidhi magari hayo, Mhe. Mtanda amewataka viongozi na watendaji wa Mkoa na Halmashauri kuhakikisha magari hayo yanatunzwa kwa mujibu wa taratibu za Serikali na yanatumika kwa malengo yaliyokusudiwa ili kuboresha huduma za sekta ya afya Mkoa wa Mara.

“Sitarajii kuona magari haya yakitumika kubeba mizigo mizito na mikaa, haya ni magari ya usimamizi na yatumike kufanya shughuli za usimamizi katika sekta ya afya” amesema Mhe. Mtanda.

Mhe. Mtanda pia amewataka wasimamizi wa magari hayo kuangalia mienendo ya madereva wao ili kujiridhisha na uendeshaji salama wa magari ya Serikali kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu za utumishi wa umma.

Aidha, Mhe. Mtanda amewakumbusha viongozi kuhusu maelekezo aliyoyatoa awali kuhusu utengenezaji wa magari ya Serikali ili yaweze kutoa huduma zilizokusudiwa.

Kwa upande wake, Katibu Tawala Msaidizi sehemu ya Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii Dkt. Zabron Masatu ameeleza kuwa magari hayo matano yanayokabidhiwa ni sehemu ya magari 33 ya  sekta ya afya yaliyotolewa na Serikali kwa Mkoa wa Mara katika mwaka huu wa fedha.

“Kwa sasa tunasubiri magari ya usimamizi ya Halmashauri tano ambayo bado hayajapokelewa na yanatarajiwa kupokelewa wakati wowote kuanzia sasa” amesema Dkt. Masatu.

Dkt. Masatu ameeleza kuwa tayari baadhi ya magari ikiwa ni pamoja na magari ya kubeba wagonjwa  kwa ajili ya Halmashauri zote za Mkoa wa Mara na Hospitali ya Rufaa ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere yamepokelewa na kukabidhiwa kwa walengwa.   

Halmashauri zilizokabidhiwa magari ya usimamizi wa sekta ya afya leo ni Halmashauri ya Wilaya ya Tarime, Halmashauri ya Wilaya ya Rorya, Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti na Halmashauri ya Wilaya ya Butiama.

Dkt. Masatu ameeleza kuwa magari hayo yataboresha ukaguzi na usimamizi wa vituo vya kutolea huduma za afya na kuwawezesha wasimamizi wa sekta ya afya ngazi za Halmashauri na Mkoa kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.   

Magari 33 yametolewa na Serikali kwa ajili ya Usimamizi wa sekta ya Afya magari 13, kwa ajili ya Mkoa, Halmashauri, Hospitali ya Rufaa ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere, Chuo cha Maafisa Tabibu Musoma na magari ya kubeba wagonjwa 20 kwa ajili ya Halmashauri tisa na Hospitali ya Rufaa ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere (Kwangwa).

 Hafla ya kukabidhi magari imehudhuriwa pia na Katibu wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Mara, Wakuu wa Wilaya, Makatibu Tawala Wasaidizi na Wakuu wa Vitengo vya Sekretarieti ya Mkoa wa Mara, Wakurugenzi wa Halmashauri na baadhi ya watendaji wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara na Halmashauri.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa