• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi: wanafunzi wote wapate chakula shuleni ifikapo Januari, 2025

Posted on: September 19th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo ameongoza kikao cha viongozi na watendaji wa Mkoa wa Mara kuhusu utoaji wa chakula shuleni na kuwataka viongozi, wazazi na wadau wote kuhakikisha kuwa wanafunzi wote wa Mkoa wa Mara wanapata chakula cha mchana shuleni kuanzia Januari, 2025.

Mhe. Mtambi ametoa agizo hilo leo wakati akizungumza katika kikao hicho na kuwataka viongozi wa Serikali wa Mkoa wa Mara kusimamia maelekezo hayo na kuhakikisha wanafunzi wote wanapata angalau mlo wa mmoja wa mchana wakiwa shuleni ili waweze kujifunza vizuri.

“Haikubaliki kuendelea kuwafanyia ukatili wanafunzi kwa kuwashindisha na njaa kwa sababu tu viongozi na wazazi tumeshindwa kutimiza wajibu wetu katika kutoa chakula shuleni” amesema Mhe. Mtambi na kuwataka wazazi na walezi wote kuchangia ili wanafunzi wapate chakula shuleni.

Mhe. Mtambi amesema chakula kinachochangiwa sio cha ziada bali ni chakula ambacho mtoto akiwa nyumbani angekula na hivyo ni wajibu wa wazazi na walezi wa wanafunzi kutoa chakula hicho ili wanafunzi wapate chakula wakiwa shuleni.

Kanali Mtambi amezitaka Halmashauri kuhakikisha kuwa shule zote zenye maeneo au mashamba zitumie maeneo hayo kulipa na kupata chakula ili kuwasaidia wazazi katika mchango wa chakula na kuwafundisha wanafunzi kwa vitendo kuhusu kilimo na shughuli za kujitegemea.

Mhe. Mtambi amewataka wadau wa elimu kuchangia kwa hali na mali ili kuhakikisha wanafunzi wote wanapata chakula shuleni na Halmashauri kutunga sheria ndogo za kusimamia utoaji wa chakula shuleni ili wazazi/walezi wanaokaidi kuchangia wachukuliwe hatua za kisheria.

Mhe. Mtambi amezitaka Halmashauri kuhakikisha kuwa chakula kinachochangwa na wazazi kinahifadhiwa vizuri na kwa usalama katika maeneo ya shule na kushughulikia wasiwasi wa wananchi kuwa chakula kinachochangwa kinatumika vibaya na walimu.

Kwa upande wake, Kaimu Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Elimu Bi. Judith Mrimi amesema programu ya chakula shuleni ni muhimu kwa ajili ya kuongeza udahili na usajili wa wanafunzi, mahudhurio, usikivu na kuinua ufaulu wa wanafunzi katika mitihani.

Bibi Mrimi amesema kwa mujibu wa mwongozo wa Kitaifa wa Utoaji wa Huduma ya Chakula na Lishe kwa wanafunzi wa Elimumsingi, wanafunzi wote wa shule za kutwa za msingi na sekondari wanapaswa kupata huduma ya chakula cha mchana shuleni.

Bibi Mrimi amesema mwongozo huo umebainisha kuwa chakula kwa ajili ya wanafunzi kitapatikana kutoka kwa Serikali kwa wanafunzi wanaosoma shule za bweni na kwa shule za kutwa michango ya chakula itatoka kwa wadau wa elimu, sekta binafsi, wabia wa maendeleo, mashamba na bustani za shule, michango ya wazazi.

Bi Mrimi amesema kuwa mwongozo huo umeainisha michango ya chakula shuleni inaweza kuwa ni pamoja na michango ya vyakula, fedha taslimu, nguvu kazi, miundombinu na michango ya uwezeshaji au kuwajengea wananchi uwezo wa kitaalamu.

Bibi Mrimi amesema Halmashauri ni moja ya wadau muhimu wa utoaji wa chakula shuleni na inatakiwa kuweka kwenye mipango yake shughuli za kuhamasisha wazazi na jamii kupitia viongozi wa mitaa au vijiji kushiriki utoaji wa chakula shuleni, udhibiti wa ubora na usalama wa chakula kwa kutoa elimu na kuandaa sheria ndogondogo za utoaji wa chakula shuleni.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa