• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi: tumieni fursa ya madaktari bingwa 40 kutibiwa

Posted on: November 29th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo ametoa taarifa kwa Waandishi wa Habari kuhusu kambi ya madaktari bingwa 40 watakaotoa huduma Hopitali ya Rufaa ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere iliyopo eneo la Kwangwa kuanzia tarehe 2-6 Desemba, 2024 na kuwataka wananchi kutumia fursa ya uwepo wa madaktari hao kutibiwa.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake, Mhe. Mtambi amesema madaktari bingwa hao wanatoka katika Hospitali za Rufaa za Mikoa ya Kanda ya Ziwa na Hospitali za Rufaa za Kanda za Bugando na Chato ambao watatoa huduma za kibingwa kwa wananchi wa Mkoa wa Mara.

“Hii ni fursa adhimu ambayo Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan imeisogeza kwa wananchi wa Mkoa wa Mara wakiitumia itawapunguzia adha ya kusafiri kufuata huduma” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi amesema huduma za madaktari hao zitakuwa na faida zaidi kwa mgonjwa kwani katika siku hizo mgonjwa anaweza kuonwa na madaktari bingwa zaidi ya mmoja ambao wanaweza kubadilishana uzoefu tofauti na akienda katika matibabu ya kawaida kama atafanikiwa kumpata daktari bingwa atakuwa mmoja.

Mhe. Mtambi amesema maganjwa yatakayotibiwa katika kambi hiyo pamoja na magonjwa ya akina mama na uzazi, magonjwa ya pua, koo na masikio, afya ya akili, magonjwa ya ndani yanayojumuisha magonjwa ya kisukari, presha, figo na kadhalika na magonjwa ya kinywa na meno.

Aidha, madaktari hao watatoa huduma za kibingwa za radiolojia, dawa za usingizi na kufanya upasuaji wa kibingwa katika Hospitali ya Rufaa ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere.  

Kwa upande wake, Katibu Tawala Msaidizi sehemu ya Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii Dkt. Zabron Masatu amesema kambi ya madaktari bingwa hao inategemewa kufanyika katika muda wa kazi kuanzia saa mbili asubuhi hadi saa 10 jioni.

Dkt. Masatu amesema malengo ya Serikali kuleta madaktari bingwa hao ni kusogeza huduma za kibingwa karibu na wananchi, kuwajengea uwezo wataalamu wa afya waliopo katika utoaji huduma za kibingwa na kuibua wagonjwa wanaohitaji huduma za kibingwa watakaotibiwa katika Hospitali za Rufaa za Kanda.

Dkt. Masatu amesema madaktari bingwa hao wanatoka Hospitali za Rufaa za Mikoa ya Kegera, Mwanza, Geita, Simiyu, Shinyanga na hospitali za Rufaa za Kanda za Chato iliyopo Mkoa wa Geita na Bugando iliyopo Mkoa wa Mwanza.

Hii ni mara ya tatu mwaka huu Serikali inaleta madaktari bingwa katika Mkoa wa Mara kwa ajili ya matatibabu ya kibingwa hata hivyo awali madaktari bingwa hao walikuwa wanaletwa katika Hospitali za Halmashauri za Mkoa wa Mara.  

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa