• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi: Mara yavuka lengo uboreshaji Daftari la Kudumu la Wapiga Kura

Posted on: September 10th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo amezungumza na waandishi wa habari kuhusiana na zoezi la uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura lililofanyika kuanzia tarehe 4 hadi 10 Septemba, 2024.

Mhe. Mtambi amemewapongeza wananchi kwa kujitokeza kwa wingi kuboresha taarifa zao na walliokuwa wanajiandikisha kwa mara ya kwanza katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura pamoja na wadau mbalimbali waliosaidia kufanikisha zoezi hilo kwa ufanisi.

 “Mpaka sasa kwa namna wananchi walivyojitokeza tumevuka lengo mara dufu na katika baadhi ya vituo tumehitajika kuongeza mashine na watumishi ili kuwahudumia watu waliojitokeza kwa wakati” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi amesema watu waliojiandikisha kwa mara ya kwanza ikiwemo vijana na watu wazima ni wengi sana na kuufanya Mkoa kuvuka maradufu lengo lake la awali la uandikishaji na uboreshaji wa taarifa katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.

Kanali Mtambi amesema zoezi hilo limefanyika kwa uwazi, utulivu na maelewano ya hali ya juu baina ya Serikali, Vyama vya siasa na wadau mbalimbali wa uchaguzi na kuchukua fursa hiyo kuwashukuru kwa ushirikiano mkubwa waliouonyesha katika kipindi chote cha uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura katika Mkoa wa Mara.

Mhe. Mtambi amesema wakati wa uboreshaji hakukuwepo wimbi la wageni kutaka kujiandikisha baada ya Mkoa wa Mara kuchukua tahadhari za mapema za kudhibiti watu wasiotambulika kujiandikisha kwa kutoa elimu kwa wadau wote ili kusaidiana katika kuwabaini watu wanaopaswa kuboresha taarifa zao.

Kwa upande wake, Mratibu wa Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Uchaguzi Mkoa wa Mara Bwana Dominicus Lusasi amesema mwitikio wa wananchi katika vituo vya kuboreshea taarifa na hususan katika maeneo ya pembezoni mwa miji ambapo kuna makazi mapya ni mkubwa sana na kulazimisha kuongezwa kwa vituo, mashine na watumishi ili kuwahudumia wananchi.

Bwana Lusasi amesema kutokana na udhibiti uliofanyika katika maeneo ya mpaka, Mkoa umeandikisha Watanzania waliokuwa na sifa za kuandikishwa na kuvipongeza vyama vya siasa kwa kusimamia kwa ukaribu na kutoa mrejesho kwa wakati wanapobaini kasoro yoyote katika zoezi hilo.

Bwana Lusasi ameipongeza Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) kwa kuratibu vizuri zoezi hilo jambo ambalo limeurahisishia Mkoa katika usimamizi wa zoezi kwa kiasi kikubwa na kuwashukuru wasimamizi wa zoezi la uboreshaji katika majimbo na kata ambao wamesimamia zoezi hilo kwa ufanisi.  

Kwa upande wake, Bi. Dotto Kulwa Paulo mwanafunzi wa Kidato cha nne katika Shule ya Sekondari ya Bweri amesema yeye amejiandikisha kwa mara ya kwanza kwa kuwa ana umri wa miaka 18 kwa sasa na anategemea atakitumia kitambulisho hicho kwa ajili ya kupiga kura wakati wa uchaguzi mkuu wa  mwaka 2025.

Bi. Dotto amesema watu wengi wamejitokeza katika kituo cha Shule ya Sekondari Bweri muda mwingi wa uandikishaji na leo watu ni wengi zaidi kwa kuwa wanaelewa kuwa leo ndio mwisho wa zoezi hili kwa Mkoa wa Mara.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa