• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi: katatueni kero za wananchi

Posted on: April 26th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Mtambi tarehe 25 Aprili, 2024 amefunga mafunzo ya Maafisa Tarafa na Watendaji wa Kata yaliyoandaliwa na Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na kuwataka watumishi hao kuwasikiliza, kushughulikia na kutatua kero za wananchi katika maeneo yao.

“Wasikilizeni wananchi na kuchukua hatua stahiki kutatua kero hizo na kama kuna jambo hulielewi uliza wenzio na viongozi wa juu zaidi na kama linakushinda mwelimishe mwananchi kwenda ngazi inayofuata” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi amewataka Watendaji wa Kata kuwasaidia wananchi kwa kutambua mahitaji na mategemeo halisi ya wananchi na kuyaingiza katika Mpango wa Maendeleo ya Kata na baadaye uingizwe katika Mpango wa Maendeleo ya Halmashauri.

Kanali Mtambi amewataka maafisa hao kusimamia miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika maeneo yao kwa weredi kwani Serikali inapeleka fedha nyingi katika Tarafa na Kata hapa nchini ili kuboresha huduma za jamii kwa wananchi wake.

“Mhakikishe kuwa fedha zilizotolewa zinatumika kufanyakazi iliyokusudiwa, kusimamia uchaguzi wa maeneo ya kujenga miradi na thamani halisi ya miradi hiyo ili kutoa taarifa kwa wananchi “ amesema Mhe. Mtambi.

Aidha, amewataka kusimamia utunzaji wa mazingira kwa kupanda miti, kusimamia mpango wa matumizi sahihi ya ardhi, kupambana kutokomeza vitendo vya ukatili wa kijinsia katika jamii, kukemea vitendo vya wananchi kujichukulia sheria mkononi na kukemea kilimo cha bangi katika maeneo yao.

Kanali Mtambi amewataka kuwahamasisha wananchi kushiriki kikamilifu uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa mwaka 2024 na Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 na hususan katika zoezi la uboreshaji wa daftari la wapiga kura litakalofanyika hivi karibuni.

Mhe. Mtambi amewataka kuanza maandalizi yam bio za Mwenge wa Uhuru katika maeneo yao ambapo Mkoa wa Mara utapokea Mwenge wa Uhuru tarehe 26 Julai, 2024 hadi tarehe 3 Agosti, 2024 utakapoukabidhi Mkoa wa Simiyu kuendelea na mbio zake.

Kwa upande wake, Mkurugenzi kutoka Ofisi ya Rais, TAMISEMI Bwana Ibrahim Minja amesema jumla ya Maafisa Tarafa 300 na Watendaji wa Kata 2,260 wamepatiwa mafunzo katika mikoa 16 ya Tanzania Bara tangu mafunzo hayo yalipoanza kutolewa.

Bwana Minja amesema lengo la TAMISEMI ni kutoa mafunzo hayo ya kuwajengea uwezo Maafisa Tarafa na Watendaji wa Kata wa Mikoa yote kabla ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa mwaka 2024 kwa kuwa hawa ndio viongozi wanaotekeleza majukumu yao karibu na wananchi.

 Mafunzo haya yalifunguliwa tarehe 24 Aprili, 2024 na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Gerald Musabila Kusaya na kuendeshwa na wataalamu kutoka Chuo cha Serikali za Mitaa Hombolo na Chuo cha Utumishi wa Umma.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa