• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi azitaka Halmashauri kutenga bajeti ya Elimu ya Watu Wazima

Posted on: September 20th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo amewaongoza wananchi katika kilele cha maadhimisho ya wiki ya Elimu ya Watu Wazima, Elimu Maalum na Elimu Nje ya Mfumo Rasmi yaliyofanyika katika uwanja wa Right to Play, Wilaya ya Serengeti na kuzitaka Halmashauri kutenga bajeti ya kutosha kwa ajili ya Elimu ya Watu Wazima.

“Mimi nitafuatilia kuhakikisha Halmashauri zote zinatenga bajeti inayotosheleza shughuli za Elimu ya Watu Wazima ili kutekeleza majukumu ya Halmashauri katika Elimu ya Watu Wazima kwa ufanisi” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi amewataka wazazi kuhakikisha kuwa watoto wao wanaenda shule na wanasoma kwa bidi na kutoa onyo kwa wazazi ambao wanagoma kuchangia chakula cha watoto shuleni na kuwatahadharisha kuwa Serikali itawachukulia hatua kali za kisheria wazazi wote ambao hawachangii chakula cha wanafunzi shuleni.

Kanali Mtambi amewataka wazazi na walezi kujidhatiti katika kulea watoto wao ikiwa ni pamoja na kuhakikisha wanapata chakula cha mchana wakiwa shuleni ili waweze kujifunza vizuri na kuacha kuwafanyia ukatili wa kuwashindisha njaa wanafunzi muda wote wanapokuwa shuleni.

Mhe. Mtambi ametumia muda huo pia kuzungumza na wanafunzi na kuwataka kuzingatia masomo na kusoma kwa bidi na kuacha mara moja kufanya tabia mbaya za utoro na utovu wa nidhamu  na mambo yasiyofaa wakiwa shuleni.

Mhe. Mtambi amesema elimu ya watu wazima ni jitihada za Serikali za kuhakikisha watu wote wanapata elimu bila kujali sehemu walipo, hali zao na uchumi wao na amewataka wananchi kutumia fursa hiyo  kujiendeleza na kujifunza ujuzi mpya kila wakati ili waweze kuboresha maisha yao na familia zao.

Mhe. Mtambi amewapongeza wananchi wa Wilaya ya Serengeti kwa kujitokeza kwa wingi katika maadhimisho hayo na kuwataka kushiriki kikamilifu katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika hapa nchini tarehe 27 Novemba, 2024.  

Kwa upande wake, Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Elimu na Mafunzo Bwana Makwasa Bulenga amesema maadhimisho ya Juma la Elimu ya Watu Wazima na Elimu Nje ya Mfumo Rasmi yanalengo la kuomarisha utaratibu, usimamizi na kutathmini maendeleo ya utekelezaji wa shughuli za elimu.

Bwana Bulenga amesema mataifa mbalimbali duniani wanachama wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi, Utamaduni (UNESCO) huungana katika kupima na kutafakari mafanikio na changamoto zilizopo katika utoaji wa elimu ya watu wazima na elimu nje ya mfumo rasmi yenye adhma ya kufuta ujinga, umaskini na maradhi.

Bwana Bulenga amesema maadhimisho haya hufayika kila mwaka tarehe 1-8 Septemba katika Mikoa na Halmashauri kwa kushirikiana na wadau mbalimbali na kauli mbiu ya mwaka huu ni “Ujumuishi katika Elimu bila ukomo kwa Ujuzi, Ustahimilivu, Amani na Maendeleo” 

Bwana Bulenga amesema katika Mkoa wa Mara, Mpango wa Elimu ya Msingi kwa Walioikosa (MEMKWA) una wanafunzi 2,463 ambapo wavulana ni 1,292 na wasichana ni 1,171 wanaosoma katika shule na vituo 127.

Bwana Bulenga amesema Mpango wa Uwiano kati ya Elimu ya Watu Wazima na Jamii (MUKEJA) ambao unawahusisha watu wazima kuanzia miaka 18 na kuendelea unatekelezwa katika vituo 69 yenye wanakisomo 1,357 ambapo huhudisha shughuli za ujasiriamali, kilimo, ufugaji, kilimo pamoja na kujifunza stadi za kusoma, kuandika na kuhesabu kwa wasiojua stadi hizo.

Bwana Bulenga amesema kuwa Mkoa wa Mara una vituo nane katika Halmashauri nane vyenye wanafunzi wakike 190 waliorudi shule baada ya kukatiza masomo katika mfumo rasmi kutokana na sababu mbalimbali.

Bwana Bulenga ameyataja mafanikio kuwa ni pamoja na wanafunzi wa MEMKWA 399 waliofanya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi na wanafunzi 310 walifaulu na kuendelea na masomo ya sekondari na kati ya wasichana 59 waliofanya mtihani wa kidato cha nne, wasichana 16 walifaulu na kuendelea na masomo ya kidato cha tano na sita.

Katika maadhimisho hayo, Mkuu wa Mkoa ametembelea mabanda ya maonyesho ya shughuli mbalimbali za elimu na kutoa zawadi kwa wanafunzi, walimu na shule zilizofanya vizuri katika maeneo mbalimbali.

Maadhimisho ya wiki ya Elimu ya Watu Wazima yamehudhuriwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara, Wakuu wa Wilaya za Mkoa wa Mara, Kamati ya Usalama ya Wilaya ya Serengeti, Maafisa kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, viongozi na watendaji wa Halmashauri, wanachi na wanafunzi.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa