• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi azindua zoezi la ugawaji wa fidia Nyatwali

Posted on: September 6th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Evans Alfred Mtambi leo tarehe 5 Septemba, 2024 amezingua zoezi la utoaji wa fidia kwa wananchi wa Kata ya Nyatwali, Wilaya ya Bunda wanaohama kupisha upanuzi wa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti (SENAPA).

Akizungumza katika uzinduzi huo, Mhe. Mtambi amesema Serikali imeruhusu wananchi hao kupata nyongeza ya fidia yao kwa asilimia 7 baada ya malipo hayo kuchelewa baada ya tathmini ya eneo hilo kukamilika kutokana na sababu mbalimbali na kuwahamasisha kuondoka mapema baada ya kupata malipo yao.

“Ni vizuri mkipata pesa ya fidia kabla hamjaanza kufanya mambo mengine muondoke mapema katika eneo hili kabla ya fedha mnazopata hamjatumia kwenye mambo mengine yasiyo na msingi” amesema Mhe. Mtambi.

Amewataka viongozi wa eneo hilo kuonyesha mfano kwa kuanza kuondoka mapema na kuzitaka familia kujadili kwa undani namna ya kwenda kujenga familia zao katika maeneo mengine watakayoamua kwenda kuanzisha maisha yao.

Mhe. Mtambi amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa kipaumbele cha malipo ya fidia kwa wananchi wa Kata ya Nyatwali na kuwawezesha wananchi hao kwenda kuishi maisha yao katika mazingira salama mbali na wanyama wanaotoka katika hifadhi.

“Hili ni eneo la mapito ya asili ya wanyama na ambalo lina manufaa makubwa katika ikolojia na fursa mbalimbali za utalii katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na Ziwa Victoria” amesema Mhe. Mtambi.

Kwa upande wake, Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini Mhe. Robert Maboto ameipongeza Serikali kwa kukamilisha mchakato wa malipo na kuiomba Serikali kutoa elimu ya kutosha ya namna zoezi la ulipaji wa fidia litakavyofanyika.

“Wananchi hawa wapo tayari kusikiliza maelekezo ya Serikali kuhusiana na zoezi hili tuwaeleweshe vizuri wananchi ili kuondoa malalamiko ya wananchi hapo baadaye” Mhe. Maboto.

Kwa upande wake, mwananchi wa Mtaa wa Kariakoo katika Kata ya Nyatwali amesema Bibi Mgesi Kisuka Machira ameishukuru Serikali kwa kutoa malipo hayo waliyokuwa wanayasubiri kwa muda mrefu na kuahidi atahama eneo hilo mapema iwezekanavyo.

“Tunamshukuru Rais kwa kutoa malipo ya kuhamishwa, kero za wanyama waharibifu tutaondokana nazo ikiwemo kuvamiwa na mamba, kiboko, tembo na wanyama wengine mara kwa mara” amesema Machira.

Bibi Machira ambaye ndiye amekabidhiwa Washima amesema amefurahia kwa kuwa Serikali imewaruhusu kwenda na vitu vyote walivyokuwa navyo ikiwemo matofali, mabati na miti ambavyo watavitumia huko wanakoenda.

Zaidi ya wananchi 3,500 wa Kata ya Nyatwali wanategemea kulipwa fidia na Seriklai kupitia Mamlaka ya Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) ambapo jumla ya shilingi 45.9 kimetengwa kwa ajili ya malipo ya wananchi kutokana na eneo hilo kupitiwa na wanyamapori kutoka SENAPA wakati wa kiangazi wanapokwenda kunywa maji Ziwa Victoria katika ghuba ya Speke.  

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa