• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi awataka wananchi kutatua changamoto kwa amani

Posted on: February 24th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi akiambatana na Kamati ya Usalama ya Mkoa wa Mara ametembelea eneo lenye mgogoro wa ardhi katika mpaka wa Kata ya Mwema na Regicheri, Wilaya ya Tarime na kuwataka wananchi kujifunza kutatua changamoto zao kwa amani.

“Sio kila changamoto inahitaji utatuzi wa kutumia nguvu na mapanga, changamoto nyingine zinazungumzika kwa amani na utulivu na inapatikana suluhu ya kudumu” amesema Mhe. Mtambi na kuongeza kuwa “hapa hamna mshindi wala bingwa katika mgogoro huu”.  

Mhe. Mtambi amewataka wananchi kuhakikisha kuwa mgogoro huu unatatuliwa kwa amani na utulivu na kuwahakikishia wakiendelea na mgogoro huo atatoa kipande kinachogombewa kwa uongozi wa JKT ili wenyemashamba katika eneo hilo wafanye kazi chini ya uongozi wa kijeshi.

Mhe. Mtambi amemwagiza Kamishana Msaidizi wa Ardhi Mkoa wa Mara kutambua mpaka wa Kata hizo na kuuangalia mpaka wa Inglam uliowekwa na Serikali ya Wakoloni sambamba na utambuzi wa wamiliki halali wa mashamba katika eneo linalogombewa.

“Baada ya kukamilisha utambuzi wa mipaka na wamiliki wenyemashamba katika eneo linalogombewa nitakuja kutoa maamuzi ya Serikali kuhusu mgogoro huu” amesema Mhe. Mtambi na kuwataka wananchi ambao hawana mashamba katika eneo hilo kuacha kuchochea mgogoro huo.  

Mhe. Mtambi amemtaka Bwana Laurent Nyablanketi mfanyabiashara anayekodisha mashamba katika eneo hilo kuacha kuendelea kuchochea mgogoro huo na kuendelea kufanyabiashara zake katika eneo hilo kwa amani.  

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Tarime Meja Edward Gowele amesema baada ya kuibuka mgogoro kwa siku za hivi karibuni alitoa maelekezo ya wananchi kuacha kufanya maendelezo yoyote katika eneo lenye mgogoro hadi hapo mgogoro huo utakapotatuliwa.

“Hii ilitokana na baadhi ya sababu za kuibuka kwa mgogoro katika eneo hili kwa wakati huu ni baada ya baadhi ya wananchi kuanza kujenga nyumba katika eneo lenye mgogoro na hivyo kuendelea kuchochea mgogoro huo” amesema Mhe. Gowele.

Mhe. Gowele amesema katika eneo hilo kuna mashamba matatu yenye hati ambayo wananchi wanasema hawawatambui wamiliki wa mashamba hayo na wamiliki hao wamekuwa wakiyakodisha mashamba hayo pamoja na kuwa eneo hilo linamgogoro wa umiliki wa mashamba hayo.

Mhe. Gowele amewashukuru wazee wa mila wa koo zenye mgogoro katika eneo hilo kwa kusaidia kutuliza mgogoro wakati Serikali ikitafuta suluhisho la kudumu la mgogoro huo.

Mgogoro huo umedumu takribani miaka 30 ukiibuka na kutulia na unazihusisha koo za Wanchari na Wakira katika vijiji vya Remugwe na Kolotambi katika kata za Mwema na Regicheri, Tarafa ya Sirari, Wilaya ya Tarime.

Katika ziara hiyo, walishiriki pia Kamati ya Usalama ya Wilaya ya Tarime, watumishi Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara na baadhi ya viongozi na maafisa wa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa