• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi awataka wakandarasi wa umeme kukamilisha miradi kwa wakati

Posted on: September 14th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo tarehe 13 Septemba, 2024 ameongoza hafla fupi ya kuutambulisha mradi wa Wakala wa Umeme Vijijini (REA) utakaotekelezwa katika vitongoji 148 katika Mkoa wa Mara na kuwataka wakandarasi kukamilisha miradi kwa wakati.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mhe. Mtambi amemtaka Mkandarasi wa mradi huo Daimon Company Limited pamoja na wakandarasi wengine waliopewa zabuni za kutekeleza miradi mbalimbali ya Umeme katika Mkoa wa Mara kukamilisha miradi hiyo kwa wakati.

“Umeme ni maisha, umeme ni maendeleo, Mheshimiwa Rais amedhamiria kuwaletea umeme wananchi wa Mkoa wa Mara maisha bora na maendeleo kwa njanya nyingi ikiwemo umeme, mlioaminiwa na kupewa miradi hii hakikisheni mhakikishe mnafanya kazi kama inavyotakiwa” amesema Mhe. Mtambi.  

Mhe. Mtambi amesema katika upande wa huduma za umeme Mkoa wa Mara upo vizuri ambapo vijiji vyote 459 vimepata huduma ya umeme, aidha, Mkoa una vitongoji 2,503 na kati ya hivyo vitongoji 899 tu havina umeme mpaka sasa na baadhi yake miradi ya ufungaji wa umeme inaendelea.  

Mhe. Mtambi amesema mbali ya mradi mpya unaotambulishwa katika hafla hiyo, kuna miradi mingine inayoendelea katika Mkoa wa Mara kwenye vitongoji 470 yenye thamani ya shilingi bilioni 90 na kwa sasa miradi hii ipo katika hatua mbalimbali za ukamilishaji wake.  

“Huyu mkandarasi mpya anayetambulishwa leo yeye atafunga umeme kwenye vitongoji 148 na kwa kasi ninayoiona ni matumaini yangu kuwa muda sio mrefu vitongoji vyote vya Mkoa wa Mara vitakuwa na huduma ya umeme” amesema Mhe. Mtambi.

Kwa upande wake, Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Wakala wa Umeme Vijijini (REA) Mhandisi Ernest Makare amesema wapo Mkoani Mara kwa ajili ya kuutambulisha mradi utakaotekelezwa katika vitongoji 148 na mkandarasi mzawa Daimon Company Limited ambao unaanza kutekelezwa rasmi kuanzia tarehe 13 Septemba, 2024.

Mhandisi Makare amesema katika mradi huo, mkandarasi anatarajiwa kujenga transforma 48 katika eneo la kilomita 296 ambazo zitawanufaisha wananchi zaidi ya 5000 kwa gharama ya bilioni 18.6 ambazo zitatumika katika kutekeleza mradi huo.

Mhandisi Makare amewathibitishia wadau walioshiriki katika hafla hiyo kuwa kuwa REA itamsimamia mkandarasi na kuhakikisha anatekeleza mradi huo kwa haraka ili wananchi waweze kupata huduma za umeme katika maeneo hayo.  

 Hafla hiyo ilifanyika katika ukumbi wa uwekezaji uliopo Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara na kuhudhuriwa na viongozi wa REA na TANESCO Mkoa wa Mara, mkandarasi na baadhi ya watumishi kutoka TANESCO, REA na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa