• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi awataka wahitimu JKT kuyaishi mafunzo yao

Posted on: September 9th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo amefunga rasmi Mafunzo ya Operesheni Miaka 60 ya Muungano kwa mujibu wa sheria yaliyofanyika na katika kikosi cha 822 JKT Rwamkoma, Wilaya ya Butiama na kuwataka wahitimu kuyaishi kwa vitendo mafunzo hayo.

Akizungumza mara baada ya kukagua gwaride, kuangalia vikundi vya maonyesho na kutoa zawadi kwa wahitimu waliofanya vizuri katika vipengele mbalimbali, Mhe. Mtambi amewata wahitimu hao kutumia ujuzi na maarifa waliyofundishwa kwa faida yao na jamii kwa ujumla.

“Katika mafunzo haya mmejifunza mambo mengi sana ambayo mkiyaishi kwa vitendo yanaweza kubadilisha maisha yenu na maisha ya watu wengi wanaowazunguka, hivyo ni jukumu lenu kuyaishi mafunzo haya kwa vitendo” amesema Mhe. Mtambi.

Kanali Mtambi amewataka wahitimu wa mafunzo hayo kuwa mabalozi wazuri wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT)  na kuzingatia mshikamano na upendo kwa watu wote bila kujali tofauti za kabila, dini na itikadi za kisiasa.

Mhe. Mtambi amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuwezesha kufanyika kwa mafunzo hayo muhimu kwa maendeleo ya vijana na kuwapongeza vijana hao kwa uvumilivu na ustahimilivu uliowasaidia kukamilisha mafunzo yao.

Mhe. Mtambi amewataka wahitimu wa mafunzo hayo kukiishi kiapo cha utii walichokitoa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kuyaishi mambo manne ya kijana wa JKT waliyoyasoma katika kiapo chao.

Kwa upande wake, Mkuu wa Kikosi 822 JKT Rwamkoma Kanali Gaudensia Joseph Mapunda ameeleza kuwa mafunzo hayo yaliyofungwa leo yameanza tarehe 19 Juni, 2024 na yamefanyika kwa wiki 12.

Akizungumza kabla ya kuwakaribisha viongozi kuongea, Kanali Mapunda amesema lengo la mafunzo hayo kwa vijana ni kuwajengea uwezo na kuwapa mafunzo ya uzalendo na utaifa.

Kanali Mapunda amesema jumla ya vijana 1,133 walipokelewa katika kikosi hicho wakati wa kuanza mafunzo ambapo  vijana 1,122 wamehitimu mafunzo yao huku vijana wakiume 11 hawakufanikiwa kuhitimu kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo utoro.  

Kanali Mapunda amewashukuru viongozi wa Serikali, vyama vya siasa, viongozi wa kimila na dini, wazazi, walezi na wananchi waliojitokeza kushiriki katika ufungaji wa mafunzo hayo.    

Kwa upande wake, Mwakilishi wa Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Kanali Amos Gerald Mollo amesema amewataka wazazi na walezi kuwaruhusu vijana kujiunga na mafunzo hayo ili kujenga Taifa lenye vijana waliotayari kulitumikia.

Kanali Mollo amewataka vijana waliohitimu mafunzo hayo kulinda afya zao kwa kula vyakula sahihi, kufanya mazoezi na kuepuka matumizi ya madawa ya kulevya na kuepuka makundi mabaya katika jamii. 

Kanali Mollo amewataka wahitimu hao kusoma kwa bidi katika mafunzo ya vyuo wanayoenda na kuwa mfano bora katika kulitumikia Taifa.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Butiama Mhe. Moses Ludoviko Kaegele amewataka wahitimu wa mafunzo hayo kwenda kupambana na umaskini kupitia mafunzo ya ujasiriamali waliyopata katika kikosi hicho.

Mhe. Kaegele amewataka vijana hao na wananchi waliohudhuria ufungaji wa mafunzo hayo kwenda kujiandikisha katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura na kushiriki uchaguzi wa Serikali za Mitaa na uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 ili kuwapata viongozi bora.

Wakisoma risala yao kwa mgeni rasmi, wahitimu wa kikosi hicho wamesema katika mafunzo hayo yamejifunza mambo mbalimbali ikiwemo uzalendo kwa Taifa, ujasiliamali, kilimo, ufugaji na kupata mafunzo ya awali ya kijeshi.

Wahitimu hao wameliomba JKT kuimarisha upatikanaji wa maji wakati wa mafunzo kwa kuweka matanki makubwa ya maji katika eneo hilo ili kupunguza changamoto ya kukosekana kwa maji.

 Kikosi cha JKT 822 kilianzishwa mwaka 1970 baada ya kuhamisha kikosi cha JKT kilichokuwepo Mwanza na kwa sasa kipo katika eneo la Rwamkoma na kina ukubwa wa ekari zaidi ya 1,000 na kina vikosi viteule vinne ikiwa ni pamoja na Kiteule Kanda ya Ziwa (Mwanza), Kiteule Tarime, Kiteule Bulamba na Kiteule Nanenane katika eneo la Nyakabindi Mkoa wa Simiyu. 

Ufungaji wa mafunzo hayo umehudhuriwa pia na Mwakilishi wa Mkuu wa Majeshi, Kamati ya Usalama ya Mkoa na Wilaya ya Butiama, viongozi wa Halmashauri ya Butiama, Chifu Japhet Wanzagi kiongozi wa Kabila la Wazanaki, viongozi wa vyama vya siasa, dini na vijiji vinavyoizunguka JKT Rwamkoma.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa