• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi awataka wadau kuhamasisha amani

Posted on: October 8th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo ameongoza kikao cha wadau wa uchaguzi kuhusiana na maandalizi ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa mwaka 2024 katika ukumbi wa Uwekezaji na kuwataka wadau wa uchaguzi kuhakikisha kuwa uchaguzi wa Serikali za Mitaa unafanyika kwa amani na utulivu.

Akizungumza katika kikao hicho, Mhe. Mtambi amewataka wadau wote kushiriki kikamilifu katika kuwahamasisha wananchi kushiriki katika matukio muhimu ya uchaguzi kwa amani na kufuata miongozo inayotolewa na wasimamizi wa uchaguzi.

“Katika uchaguzi huu tunahitaji amani na utulivu, vyama na wagombea wanadi sera zao na kuwashawishi wananchi wawachague na Serikali ya Mkoa tutahakikisha tunaweka mazingira mazuri ya uchaguzi” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi amesema zoezi la uandikishaji wa wapiga kura litafanyika kuanzia tarehe 11 hadi 20 Oktoba, 2024 na kuwataka wananchi kujitokeza kwa wingi ili wapate haki ya kupiga na kupigiwa kura kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa maana wasipojiandikisha hawataweza kupiga kura.

Kanali Mtambi amesema sifa za mtu anayepaswa kujiandikisha ni; awe raia wa Tanzania mwenye umri wa miaka 18 au zaidi, mkazi wa Mtaa, Kijiji au Kitongoji ambapo uchaguzi unafanyika na kuongeza kuwa orodha ya wapiga kura itabandikwa kwenye mbao za matangazo na Msimamizi wa Uchaguzi tarehe 21 Oktoba, 2024 ambapo watakaoonekana kwenye orodha hiyo ndio watakaoruhusiwa kupiga kura.

Mhe. Mtambi amesema zoezi la kuchukua na kurejesha fmu za kugombea nafasi za uongozi litafanyika tarehe 01-07 Novemba, 2024 na kuzitaja nafasi zonazogombewa kuwa ni Mwenyekiti wa Mtaa, Wajumbe wa Kamati ya Mtaa (kundi mchanganyiko) na kundi la wananwake kwa Halmashauri za Miji na Manispaa.

Kwa Halmashauri za Wilaya, nafasi zinazogombewa ni Mwenyekiti wa Kijiji, Wenyeviti wa Vitongoji vilivyomo katika eneo la kijiji, wajumbe wa Halmashauri ya Kijiji (kundi mchanganyiko) na kundi la wanawake.  

Mhe. Mtambi amesema zoezi la uteuzi wa wagombea litafanyika tarehe 8 Novemba, 2024 na viongozi wa vyama vya siasa wanatakiwa kuwasilisha ratiba ya mikutano ya kampeni tarehe 14 Novemba, 2024 na kampeni za uchaguzi zitafanyika tarehe 20 Novemba, 2024 hadi tarehe 26 Novemba, 2024.

Mhe. Mtambi amezitaja sifa za mpiga kuwa kuwa ni Raia wa Tanzania, mwenye umri wa miaka 18 au zaidi, mkazi wa Mtaa, Kijiji, au Kitongoji ambapo uchaguzi unafanyika, aliyejiandikisha kupiga kura katika Mtaa, Kijiji, au Kitongoji chake.

Kwa upande wake, Msimamizi wa Uchaguzi Mkoa wa Mara Bwana Dominicus Lusasi amesema Mkoa wa Mara una jumla ya tarafa 20, kata 178, mitaa 242, vijiji 458 na vitongoji 2,502, Wilaya sita na Halmashauri tisa.

Bwana Lusasi amesema Mkoa wa Mara unatarajiwa kuwa na wapiga kura 1,111,963 kulingana na takwimu Sensa ya Watu na Makazi yam waka 2022 zilizotolewa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS)

Bwana Lusasi amesema wakati wa uchaguzi Mkoa utakuwa na vituo vya uandikishaji 2,854 ambapo kati ya hivyo vituo 1,782 vipo kwenye majengo ya umma na vituo 1,065 havipo kwenye majengo ya umma na mkoa unatarajia kuwa na vituo vya kupigia kura 3,053 hii ni kutokana na ongezeko la vituo kwenye Halmashauri ya Mji wa Tarime.

Kauli Mbiu ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2024 ni “Serikali za Mitaa, Sauti ya Wananchi, Jitokeze Kushiriki Uchaguzi”.

Kikao hicho kimehudhuriwa pia na Viongozi wa vyama vya siasa, viongozi wa dini, wazee wa kimila na machifu, Wakuu wa Idara na Vitengo vya Sekretarieti ya Mkoa wa Mara, mashirika yasiyo ya kiserikali, waratibu wa uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa