• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi awataka vijana kushiriki uchaguzi

Posted on: November 14th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo tarehe 14 Novemba, 2024 amemwakilisha Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kufunga Kongamano la Fursa za Kiuchumi kwa vijana wa mikoa ya Mara, Simiyu na Mwanza lililofanyika katika Hoteli ya CMG, Mjini Tarime na kuwataka vijana kushiriki katika masuala ya uchaguzi.

“Tunashukuru kuwa vijana wengi mmejiandikisha katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa na kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025, ninawaomba mjitokeze kugombea nafasi mbalimbali na kupiga kura katika chaguzi hizi ili kuwachagua viongozi bora” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi amesema kujiandikisha tu bila kushiriki kupiga kura tarehe 27 Novemba, 2024 haitakuwa na maana yoyote ile na kuwataka kujitokeza kwa wingi kuchagua viongozi watakaosimamia maendeleo ya maeneo yao.

Mhe. Mtambi amewataka vijana kuendelea kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kazi nzuri anazoendelea kuzifanya katika sekta mbalimbali hapa nchini na kuwataka vijana kumuunga mkono kwa kufanya kazi kwa bidi ili kujiletea maendeleo yao.

Akizungumza katika Kongamano hilo, Mkuu wa Wilaya ya Musoma Mhe. Juma Chikoka amesema sifa kubwa ambayo vijana wanapaswa kuwa nazo ni kujiamini, uthubutu na kuchungulia fursa na kuzifanyia kazi na amewapongeza vijana wote walioshiriki katika kongamano hilo.

Mhe. Chikoka amesema mwaka huu uchaguzi upo mikononi mwa vijana ndio watakaoamua hatma ya jamii zetu kwa kwenda kupiga kura na kuhakikisha amani na utulivu katika maeneo yote ili kusiwe na hofu ya wananchi kujitokeza kwenda kupiga kura.

Kwa upande wake, Mbunge wa Tarime Mjini Mhe. Michael Kembaki amesema Chama cha Mapinduzi kimejipanga vizuri katika Mkoa wa Mara na kina uhakika wagombea wake wengi watashinda katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka huu.

“Tutapita Mtaa kwa Mtaa, Kijiji kwa Kijiji, Kitongoji kwa Kitongoji na nyumba kwa nyumba kufanya kampeni na kuwahamasisha watu waliojiandikisha kupiga kura” amesema Mhe. Kembaki.

Mhe. Kembaki amewataka vijana hao kukisaidia Chama kufanya kampeni na kuwahamasisha vijana wenzao kuwachagua viongozi bora watakaosaidia kuleta maendeleo katika maeneo yao.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa