• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi awapongeza wanamara kwa ukomavu wa kisiasa

Posted on: November 27th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo amepiga kura kuwachagua viongozi wa Serikali ya Mtaa katika kituo kilichopo Ofisi ya Kata Mukendo, Manispaa ya Musoma na kuwapongeza wananchi wa Mkoa wa Mara kwa ukomavu wa kisiasa na kuwataka wajitokeze kwa wingi kupiga kura.

Akizungumza mara baada ya kupiga kura Mhe. Mtambi amesema katika kampeni za uchaguzi wa Serikali za Mitaa wananchi wameonyesha ukomavu wa kisiasa uliosababisha kampeni kufanyika kwa amani na utulivu na hamna malalamiko ya vyama au wagombea kufanyiwa fujo wakati wa kampeni.

“Ninawapongeza wananchi wa Mkoa wa Mara kwa ukomavu mkubwa wa kisiasa waliouonyesha katika kipindi chote cha kampeni na ninawakumbusha kujitokeza kwa wingi kupiga kura ili kuwachagua viongozi wanaowataka” amesema Mhe. Mtambi.

Kanali Mtambi amevitaka vyama vya siasa na wanachama wao kuheshimu na kuzifuata kanuni za uchaguzi wa Serikali za Mitaa ambazo walishiriki kuzitunga na kama kuna malalamiko yoyote wanaweza kuwasilisha malalamiko hayo sehemu zinazohusika kwa mujibu wa kanuni za uchaguzi.

Aidha, Mkuu wa Mkoa amepiga marufuku mikusanyiko isiyo ya lazima wakati huu wa uchaguzi na kuwataka wananchi kuhakikisha kuwa baada ya kupiga kura wanaenda kuendelea na shughuli zao za kila siku.

Mhe. Mtambi amewaonya watu wanaopanga kufanya vurugu na kuahidi kuwa Kamati ya Usalama ya Mkoa wa Mara na wananchi wa Mkoa wa Mara hawatamvumilia mtu yoyote atakayeanzisha fujo katika kipindi hiki na kuwahakikishia wananchi kuwa Serikali itawachukulia hatua za kisheria watu wote wanaoanzisha vurugu wakati huu.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Musoma Mhe. Juma Chikoka akizungumza katika eneo hilo amewaomba wananchi wa Wilaya ya Musoma kujitokeza kwa wingi kushiriki uchaguzi na kuwahakikishia usalama wao wakati wote wa uchaguzi.

Mhe. Chikoka pia amewataka wananchi kuachana na mikusanyiko isiyo ya lazima na kutoa taarifa kwa viongozi wanapohisi kuna uwezekano wa uvunjifu wa amani katika maeneo yao.

Vituo vya kupigia kura vimefunguliwa saa mbili kamili asubuhi na vinategemewa kufungwa saa 10 jioni na baada ya kupiga kura wananchi wanashauriwa kuondoka katika eneo la kituo cha kupiga kura kwa utulivu na amani.

Leo ni siku ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa ambapo wananchi wanachagua viongozi mbalimbali wakiwemo wenyeviti wa Mitaa/Vijiji, wajumbe wa serikali ya mtaa/kijijji, wenyeviti wa vitongoji na kauli mbiu ya mwaka huu ni Serikali za Mitaa, Sauti ya Wananchi, Jitokeze kushiriki Uchaguzi.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa