• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi awaongoza wananchi kusikiliza hotuba ya miaka 60 ya Muungano

Posted on: April 26th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Afred Mtambi tarehe 25 Aprili, 2024 amewaongoza wananchi wa eneo la Nyasho, Manispaa ya Musoma katika kufuatilia hotuba ya Miaka 60 ya Muungano iliyotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Akizungumza kabla ya kuanza kwa hotuba hiyo, Mhe. Mtambi amewataka wananchi wa Mkoa wa Mara kujivunia mafanikoa ya Muungano kwa kuwa Mwasisi wa Muungano Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ambaye pia ni Baba wa Taifa letu ametokea Mkoa wa Mara.

“Tunatakiwa tutembee kifua mbele, tuwe na fahari, tujisikie vizuri sana kwa sababu mwasisi mmoja wapo wa Muungano ni Mwanamara----kwa hiyo Mara ni waasisi wa Muungano wa Tanzania, sisi ni kati ya Watanzania wanaotakiwa kutembea kifua mbele kujivunia Muungano wetu” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi amesema Mkoa wa Mara ni waasisi wa Muungano wa Tanzania na kama Watanzania wengine ni sehemu ya mafanikio ya miaka 60 ya Muungano na kuwataka wananchu kuendelea kuuenzi, kuulinda na kuuishi muungano wetu kwa vitendo.

Mhe. Mtambi amekemea vitendo vya kujichukulia sheria mkononi na kukatana mapanga au kuchomana visu katika mambo ambayo yanaweza kuzungumzika au kutafutiwa suluhu nzuri ikiwemo kushtakiana kuliko kuumizana.

“Miaka sitini ya Muungano, Mara uoga sasa basi, pamekuwa na matukio mengi Mkoa wa Mara ya watu kupigana visu, mapanga na vitu vyenye ncha kali, huo ni uoga, mwanaume unapigana kwa panga? Ukihitilafiana na mwenzako, hatua ya kwanza ni kumfuata na kuzungumza nae sio kumchoma mwenzako na visu na kukimbia, huo ni uoga” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi ametumia muda huo pia kujitambulisha kwa wananchi wa Kata ya Nyasho walioungana nae kufuatilia hotuba hiyo na kuwaomba ushirikiano katika utekelezaji wa shughuli zake na kuwaahidi milango ya ofisi yake ipo wazi wakati wowote.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Musoma Mhe. Dkt. Khalfan Haule ameeleza kuwa Mkoa wa Mara umepiga hatua kubwa sana katika miaka 60 ya Muungano ambapo kabla ya Muungano Mkoa ulikuwa na Wilaya mbili tu Musoma na Tarime lakini kwa sasa Mkoa una Wilaya sita na Halmashauri tisa.

 Dkt. Haule amesema kwa sasa Serikali imeshatoa fedha za ujenzi wa soko la kisasa la Mkoa katika eneo la Nyasho na Stendi ya Mkoa katika eneo la Bweri ambapo miradi hiyo itakapokamilika itabadilisha sana madhari na uchumi wa Wilaya ya Musoma.

“Thamani ya miradi hii ni bilioni 14, wataalamu wameanza kupita na hatua mbalimbali za kuwapata wakandarasi wa kutekeleza miradi hiyo zinaendelea na tayari tumeshakutana na wafanyabiashara wanaofanya biashara katika maeneo haya na kuzungumza nao” amesema Dkt. Haule.

Kwa mujibu wa Dkt. Haule wafanyabiashara wa sasa wa eneo la Nyasho watahamishwa kupisha ujenzi wa mradi huo na baada ya ujenzi kukamilika watarudishwa katika soko hilo kuendelea na biashara zao katika mazingira mazuri zaidi.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mhe. Benedict Magiri ameeleza kuwa kuna mafanikio makubwa sana katika Mkoa wa Mara tangu waasisi wa Muungano walipoiunganisha Tanzania kuwa nchi moja hadi leo hii.

Mhe. Magiri ameeleza kuwa Wanamara kama watanzania wengine tuna kila sababu ya kujivunia kuwa Watanzania kwa kuwa tuna amani na uhuru wa kutosha katika mkoa wetu na nchi yetu unaotusaidia kufanya shughuli za maendeleo.  

Bwana Magiri amesema kwa kipindi hichi chote cha Muungano, kuna maboresho makubwa katika sekta mbalimbali ikiwemo elimu, usafiri, utawala na kadhalika. Maendeleo ni makubwa sana katika Mkoa wa Mara, pamoja na kuwepo na changamoto ndogondogo zinazoendelea kutatuliwa na Serikali, wananchi wenyewe na wadau wa maendeleo.

Shughuli hiyo ilihudhuriwa pia na Kamati ya Usalama ya Mkoa wa Mara, Kamati ya Usalama ya Wilaya ya Musoma, watumishi wa umma kutoka taasisi zote zilizopo Manispaa ya Musoma, wanachama wa Chama cha Mapinduzi na wananchi wa Kata ya Nyasho.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa