• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi: Awamu ya Sita imewekeza bilioni 497 za miradi ya maji Mara

Posted on: October 8th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo ameshiriki katika kipindi cha 360 kinachorushwa na Televisheni ya Clouds kuhusiana na huduma za maji na kusema kuwa Serikali imewekeza shilingi bilioni 497 katika miradi mbalimbali ya maji katika Mkoa wa Mara.

Mhe. Mtambi ametoa kauli hiyo wakati akizungumza katika kipindicha 360 kilichorushwa mubashara kutokea Chujio la Maji la Bukanga, Manispaa ya Musoma, amesema tangu iingie madarakani tayari  Serikali ya Awamu ya Sita imetoa shilingi trilioni 1.22 kwa ajili ya miradi mbalimbali ya maendeleo katika Mkoa wa Mara na kati ya miradi hiyo uboreshaji wa huduma za maji umepewa kipaumbele.

“Uwekezaji uliofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita ni mkubwa sana ukilinganisha na uwekezaji ambao umefanyika katika uboreshaji wa huduma za maji tangu nchi ilipopata uhuru” amesema Kanali Mtambi na kuongeza kuwa hivi sasa kila Wilaya ina mradi mkubwa wa maji unaoendelea.

Mhe. Mtambi amesema tangu nchi ilipopata uhuru mpaka mwaka 2021 Serikali ya awamu ya sita ilipoingia madarakani, upatikanaji wa maji katika Mkoa wa Mara ulikuwa na wastani wa asilimia 59.1 lakini kwa sasa ni wastani wa asilimia 74 na kuongeza kuwa miradi inayoendelea ikikamilika Mkoa utakuwa na hali nzuri zaidi katika upatikanaji wa maji.  

Mhe. Mtambi ameitaja miradi mikubwa inayotekelezwa kuwa ni pamoja na mradi wa Rorya- Tarime- Sirari unaotoa maji Ziwa Victoria na kwenda katika Wilaya za Tarime na Rorya wenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 134 na mradi mwingine ni mradi wa Maji wa Mgango- Kiabakari-  Butiama unaotoa maji Ziwa Victoria na kusambaza katika vijiji 39 vya Wilaya za Butiama, Bunda na Musoma kwa gharama ya shilingi bilioni 70.5.  

Mhe. Mtambi amesema kuwa hali ya upatikanaji wa maji kwenye vijiji ni asilimia 74.6 wakati mijini ni asilimia 76 na kuongeza kuwa ni matumaini yake kuwa mwishoni mwa 2025 miradi mingi inayoendelea itakuwa imekamilika na Mkoa wa Mara utafikia lengo la Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ya  mwaka 2020 katika upatikanaji wa maji.

Mhe. Mtambi amesema kwa sasa sehemu kubwa ya wananchi wa Mkoa wa Mara wanapata maji safi, salama na ya uhakika na hivyo kutumia muda mwingi kutekeleza majukumu mengine ya kiuchumi badala ya kutafuta maji.

Wakati huo huo, Mhe. Mtambi amewahamasisha watu wanaotaka faida katika uwekezaji kuwekeza mitaji yao katika katika fursa mbalimbali zilizopo katika Mkoa wa Mara.

Ameyataja maeneo yenye fursa nyingi za uwekezaji kuwa ni Ziwa Victoria katika ufugaji wa samaki katika vizimba, uwekezaji katika fukwe, usafirishaji wa majini, utalii wa kwenye maji na kuanzisha migahawa inayotembea na uwekezaji katika sekta za ufugaji.

Akizungumzia kuhusu madini, Mhe. Mtambi amesema katika Mkoa wa Mara kila Wilaya ina migodi ya madini na madini yanayopatikana kwa wingi ni dhahabu, shaba na mengine na kuwataka wawekezaji kujitokeza kwa wingi kuchangamkia fursa hizo.

Mhe. Mtambi amesema wananchi wa Mkoa wa Mara ni watu hodari sana na katika wafanyabiashara wakubwa wa nchi hii na hususan mikoa ya Kanda ya Ziwa, wananchi wa Mkoa wa Mara wanafanya vizuri sana katika nyanja zote.    

 Wengine walioshiriki kipindi hicho ambacho kilikuwa kinazungumzia huduma za maji katika Mkoa wa Mara ni Mkuu wa Wilaya ya Musoma Mhe. Juma Chikoka, Meya wa Manispaa ya Musoma Mhe. Patrick William Gumbo, Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Musoma Mhe. Benedict Magiri na viongozi wengine.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa