• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi awahamasisha waandishi kuutangaza Mkoa wa Mara

Posted on: May 17th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo ameongoza Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Mkoa wa Mara yaliyofanyika katika Hoteli ya Afrilux ,Manispaa ya Musoma na kuwataka Waandishi wa Habari kutumia maarifa yao na ubunifu kuutangaza Mkoa wa Mara.

Akizungumza wakati wa kufunga maadhimisho hayo, Mhe. Mtambi amesema taswira ya Mkoa wa Mara iliyopo nje ya Mkoa ni tofauti na hali halisi iliyopo ndani ya Mkoa wa Mara na kwamba kuna mambo mengi mazuri yaliyopo lakini hayapewi kipaumbele na Waandishi wa Habari na vyombo vya habari hapa nchini.

“Mkoa wa Mara una mambo mengi mazuri ambayo hayaandikwi ipasavyo au hayaandikwi kabisa kama vile uwepo wa asilimia kubwa ya Ziwa Victoria, Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, madini, wasomi na viongozi kutoka Mara, wakulima na wafugaji wazuri hayapewi kipaumbele kwenye vyombo vyetu vya habari” amesema Mhe. Mtambi.

Kanali Mtambi amewataka Waandishi wa Habari kuandika habari kwa kuzingatia weledi na maadili ya uandishi wa habari na uhalisia uliopo na sio kutoa habari mbaya tu kila wakati ambazo amesema hazijengi taswira nzuri ya Mkoa wa Mara kwa wadau wake waliopo ndani na nje ya Mkoa wa Mara.

Aidha, Mhe. Mtambi amewataka Watendaji Wakuu wa Taasisi na Viongozi wa Mkoa wa Mara kutoa ushirikiano kwa waandishi wa Habari ili waweze kupata taarifa kwa urahisi na kutekeleza kwa ufanisi  majukumu yao.

Kanali Mtambi ameipongeza Klabu ya Waandishi wa Habari wa Mkoa wa Mara kwa kazi nzuri inayoifanya na kumuagiza Mkurugenzi wa Manispaa ya Musoma kuitafutia kiwanja Klabu hiyo ili iweze kujenga ofisi na kuahidi kuwa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara itachangia katika ujenzi wa ofisi ya Klabu hiyo.

Aidha, Mhe. Mtambi amewataka waandishi kutumia vizuri uhuru waliopewa na kuongeza kuwa pamoja na Serikali inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwapa uhuru wa kutosha, uhuru huo umeambatana na wajibu kwa Waandishi wa Habari kufanya kazi kwa mujibu wa sheria, miongozo na taratibu za nchi.

Mkuu wa Mkoa pia amesema Serikali ipo katika hatua za mwisho kukamilisha malipo ya fidia kwa wananchi wa Kata ya Nyatwali Wilaya ya Bunda wanahama katika eneo hilo kupisha upanuzi wa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti (SENAPA).

Akisoma risala ya Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Mara, Kaimu Mwenyekiti wa Klabu hiyo Bwana Raphael Okello amemshukuru Mkuu wa Mkoa wa Mara kwa ushirikiano mkubwa aliouonyesha kwa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Mara na hususan kushiriki katika maadhimisho hayo.

Bwana Okello ameeleza kuwa Klabu yao imeanza mchakato wa kutafuta kiwanja kwa ajili ya ujenzi wa ofisi lakini inakabiliwa na uhaba wa fedha na kuiomba Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara na wadau wengine kuwasaidia kununua kiwanja hicho.

Bwana Okello amezitaja baadhi ya changamoto kuwa ni baadhi ya viongozi na watendaji wa Serikali wamekuwa hawatoi ushirikiano kwa Waandishi wa Habari katika kutekeleza majukumu yao jambo ambalo linakiuka uhuru wa kujieleza na upatikanaji wa habari.

Ameitaja changamoto nyingine kuwa ni baadhi ya Waandishi wa Habari kukosa bima ya afya na hivyo kuwawia vigumu kupata matibabu pindi wanapokuwa wameugua.

Maadhimisho hayo yamehudhuriwa pia na wadau mbalimbali wakiwemo Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Manispaa ya Musoma, Mgodi wa Barrick North Mara, Wakala wa Maji Vijijini na Mijini (RUWASA), Wakala wa Misitu (TFS), viongozi wa vyama vya siasa, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), maafisa kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.  

Kitaifa Maadhimisho ya Uhuru wa Vyombo vya Habari yalifanyika Mkoani Dodoma tarehe 03 Mei, 2024 na Mgeni Rasmi alikuwa ni Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa (Mb.).

 Kauli mbiu ya maadhimisho haya mwaka huu ilikuwa “Uandishi wa Habari na Changamoto za Mabadiliko ya Tabia Nchi”.  

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa